HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 2, 2016

MWILI WA BONDIA THOMAS MASHALI AZIKWA LEO MAKABURI YA KINONDONI JIJINI DAR

Ndugu Jamaa na Marafiki wakipokea Sanduku lenye mwili wa Marehemu,Bondia Thomas Mashali ukiwasili katika viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar Es Salaam,Marehemu Thomas Mashali ambaye mazishi yake yanatarajiwa kufanyika jioni ya leo Makaburi ya Kinondoni.Mashali alifariki mwishoni mwa wiki kwa kuuwawa na watu wasiojulikana maeneo ya Kimara,jijini Dar. Ndugu Jamaa na Marafiki wakipokea Sanduku lenye mwili wa Marehemu,Bondia Thomas Mashali ukiwasili katika viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar Es Salaam
Sehemu ya Waombolezaji wakijianda kwenda kuaga na kutoa heshima zao za mwisho .


Ndugu Jamaa na Marafiki wakitoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa Marehemu,Bondia Thomas Mashali aliefariki mwishoni mwa wiki kwa kuuwawa na watu wasiojulikana maeneo ya Kimara,jijini Dar .


Baadhi ya ndugu,jamaa na marafiki wakiwa wamejipanga mstari tayari kwa kutoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa Marehemu,Thomas Mashali mapema leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar.
Gari lililobeba mwili wa Marehemu Thomas Mashali likiwasili katika viwanja vya Leaders Club,Kinondoni jijini Dar kwa ajili ya kutolewa heshima za mwisho kwa watu mbalimbali.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad