HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 4, 2016

WANAOJICHUKULIA SHERIA MKONONI WAONYWA- JESHI LA POLISI.


Katika siku za hivi karibuni kumeendelea kuwepo kwa vitendo na tabia ya  baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga, kuwachoma moto na kuwaua  baadhi ya watu wasio na hatia pamoja na wanaoshukiwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu  jambo ambalo ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Mpaka sasa takwimu za makosa ya kujichukulia sheria mkononi yaliyoripotiwa katika vituo vya Polisi katika kipindi cha Januari hadi Agosti mwaka 2016 ni matukio  705 . Katika matukio hayo yaliyoripotiwa, Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa 393. 

 Kufuatia hali hiyo, Jeshi la Polisi nchini linatoa onyo kali kwa wote wenye tabia ya kujichukulia sheria mkononi kuacha mara moja, Aidha, kwa kuzipuuza sheria za nchi zilizopo na wakati mwingine kuzikiuka kwa makusudi na mbaya zaidi baadhi yao kufikia hatua ya kuwaua watu wasio na hatia kwa hisia. Mwananchi yeyote anapaswa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya mhalifu au mtu yeyote wanayemtilia mashaka katika maeneo yao.

Aidha, Jeshi la Polisi nchini, litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria kwa kufuatilia na kuwakamata watu wote wanaojihusisha na tabia za kujichukulia sheria mkononi. 

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa watu wote wakiwemo wenye ushawishi mkubwa katika jamii kuendelea kukemea na kutoa elimu juu ya madhara ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake wananchi kuendelea kutii na kufuata sheria za nchi zilizopo.
 Imetolewa na:
Advera Bulimba - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.        

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad