HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 29, 2016

TAASISI YA OCEAN ROAD YAFANYA MATEMBEZI YA HISANI KUCHANGIA SARATANI YA MATITI JIJINI DAR

Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Hamis Kigwangala akizungumza mara baada ya kumaliza matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti yaliyoandaliwa na Taasisi ya Saratani ya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam ambapo huu ni mwaka wa nne tokea yameanzishwa. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Mmoja ya wagonjwa ambaye amepona saratani ya matiti akitoa ushuhuda mbele ya wageni.
 Askari wakiongoza matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
TAASISI ya Saratani ya Hospital ya Ocean Road leo imefanya matembezi ya hisani kwa lengo la Kuhamasisha na kuchangia zaidi ya milioni 120 zinazohitajika kwa ajili ya kununua vifaa tiba vya chemotherapy.

Matembezi hayo yalianzia Hospitali ya Ocean road na kumalizika hapo hapo huku wakizunguka moja ya barabara za jiji la Dar es Salaam huku Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Hamis Kigwangala akiwa ni mgeni rasmi.
Matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti yaliyoandaliwa na Taasisi ya Saratani ya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam
 Wananchi waliojitokeza katika mara baada ya kumaliza matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti yaliyoandaliwa na Taasisi ya Saratani ya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad