HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 5, 2016

ELIMU YA UFUNDI IMARA YAHITAJIKA KATIKA UCHUMI WA VIWANDA.

 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo (kulia) akizindua  baraza la kwanza la wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) jijini Dar es Salaam jana. na kushoto ni Mwenyekiti nwa Bodi ya NACTE, Mhandisi Stephen Mlote.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo (kulia) akimkabidhi  nakala za jarida la   utekelzaji wa shughuli za baraza la wafanyakazi Kaimu Katibu  Mtendaji wa  Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) , Dk Adolf Rutayuga  kwenye hafla ya  uzinduzi wa baraza hilo la kwanza la  wafanyakazi  wa NACTE jijini Dar es Salaam leo Oktoba 4, 2016. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya NACTE, Mhandisi, Stephen Mlote.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo (katikati) akizungumza na wafanyakazi  wakati akizindua  baraza la kwanza la wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) , jijini  Dar es Salaam leo Oktoba 4, 2016. Kulia ni Kaimu  Katibu Mtendaji wa NACTE, Dk Adolf Rutayuga na kushoto ni Mwenyekiti nwa Bodi ya NACTE, Mhandisi Stephen Mlote.
Wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) wakimsikiliza kwa makini Naibu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo  ambaye alizindua bara za kwanza la wafanyakazi  wa NACTE jijini Dar es Salaam leo Oktoba 4, 2016.

Na Mwandishi Wetu
Taasisi  ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi  (NACTE) ina dhamana kubwa ya hatma ya Elimu ya Ufundi  nchini Tanzania, jambo linafanya  elimu ya  Ufundi kuwa ya umuhimu  hususan katika kipindi hiki ambacho agenda kuu ya Taifa ni kujenga Uchumi wa Viwanda  kwakujenga  elimu ya ufundi imara.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Elimu Sayansi na Teknlolojia, Dk Leonard Akwilapo wakati akizindua baraza la wafanyakazi wa NACTE jijini Dar es Salaam leo Oktoba 4,2014.
Dk Akwilapo alisema kuwa  agenda hiyo inabidi ichukuliwe na Baraza hili kama kigezo cha kupima utendaji wa kazi wa NACTE. 

“ Ni matumaini yangu kuwa wajumbe wote wa Barza hili tunalolizindua leo watatambua hili na kutoa mchango maridhawa katika Maendeleo ya Taifa na kufanikisha agenda ya Taifa ya “Uchumi wa Viwanda”.alisema naibu katibu mkuu huyo
Alisemama kwa sasa i uchumi wa dunia unaendeshwa katika misingi ya soko huria na Sekta yetu ya Elimu haijaachwa nyuma katika hilo. Hata hivyo kwa kiasi kikubwa utoaji wa Elimu nchini kwetu bado ni huduma.

 Hivyo basi NACTE lazima iwe makini katika kusimamia uendeshaji wa Sekta hii, kwa kuzingatia maadili ili kuondoa huo utata. Endeleeni na usimamiaji madhubuti wa Elimu ya Ufundi, msiyumbishwe na wafanyabiashara wanaotaka kuharibu mfumo wetu wa elimu. 

Matarajio yenu yaendelee kuwa ni utoaji wa elimu yenye ubora wa kiwango cha juu cha mafunzo. 
“Ni RAI yangu kwa Baraza la Wafanyakazi kusimamia hili kwa nguvu zenu zote.  Msiposimama imara mtakuta mna vyuo batili, vyuo vinavyoendesha mafunzo kiholela bila kufuata taratibu, na vitatoa wataalamu wasio na uwezo unaolingana  na kiwango cha vyeti wanavyotunukiwa. Baraza la Wafanyakazi hamtakwepa lawama katika hali kama hiyo” alisema Dk Akwilapo

Alisema kuwa uzinduzi wa baraza hilo lilikuwa ni  muhimu sana katika historia ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), hii ni kwa sababu kama taasisi mmekuwa hamna Baraza la Wafanyakazi kwa kipindi kirefu sana. Natambua kwamba kwa kipindi chote cha uhai wa taasisi tangu ilipoanza shughuli zake takribani miaka kumi na tano (15) iliyopita, mmekuwa mkiendesha shughuli zenu bila kuwa na chombo hiki. Na hiyo ni kinyume kabisa na taratibu za utawala bora. Sina budi kuwapongeza kwa kutambua hilo na kuamua sasa kuanza kutekeleza majukumu yenu kulingana taratibu.

Naibu Katibu Mkuu huyo alisema kuwa alifahamu kuwa nia na juhudi za kutaka kuunda Baraza la Wafanyakazi la Taasisi hii zilianza muda mrefu yapata miaka nane (8) iliyopita. 

Changamoto iliyokuwepo na kukwamisha uundwaji wa Baraza hili muhimu ilikuwa ni kutokuwepo kwa tawi la chama cha Wafanyakazi katika Taasisi hii. Utaratibu wa kuundwa kwa Baraza la Wafanyakazi unahitaji kuwepo na makubaliano ya pande mbili, upande wa Mwajiri kwa upande mmoja na Chama cha Wafanyakazi mahali pa kazi kwa upande mwingine. Kwa sasa hali ni tofauti kwa kuwa “TUGHE” moja ya chama cha Wafanyakazi nchini kimefanikiwa kuanzisha tawi lake hapa na hatimaye kuwezesha kuundwa kwa Baraza hili la Wafanyakazi.

“Kwa kutambua hili napenda nichukue fursa hii kulipongeza Baraza la Uongozi wa NACTE na Menejimenti yake kwa jitihada mlizozifanya kuhakikisha kuwa tawi la chama cha Wafanyakazi “TUGHE” linafunguliwa hapa na kisha kuunda Baraza hili la Wafanyakazi. Baraza ambalo kuanzia leo linakuwa rasmi”, alisema Dk Akwilapo.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi wa NACTE, Mhandisi, Stephen Mlote alitaja majukumu ya baraza la wafanyakazi kuwa ni pamoja na kuwashirikisha wafanyakazi wa NACTE katiak utekelezaji wa shughuli za NACTE kwa kushirikiana na uongozi.

Majukumu mengine ni kushauri NACTE  juu ya ufanisi wa kazi na hatua zinazofaa kuchukuliwa na kuhakikisha  kuwa huduma zitolewazo na NACTE ni za kuridhisha  na zimo  katika lengo la kujenga  Taifa.
Mwenyekiti huyo alitaja  majukumu mengine ya baraza hilo ni kushauri NACTE  juu ya mambo mengine muhimu yanayohusu  maslahi ya wafanyakazi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad