HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 9, 2016

VIONGOZI WA SERIKALI NA WANANCHI WAFURAHIA HUDUMA ZA MFUKO YA UWEKEZAJI WA UTT WAKATI WA MAONYESHO YA NANENANE LINDI.

UTT AMIS ni kampuni inayoendesha mifuko ya uwekezaji wa pamoja hapa nchini. 

Mpaka sasa inaendesha mifuko mitano ambayo ni Mfuko wa Umoja, Mfuko wa Wekeza Maisha, Mfuko wa Watoto, Mfuko wa Kujikimu na Mfuko wa Ukwasi yenye jumla ya thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 253.

Mifuko ya uwekezaji wa pamoja ni fursa mbadala inayowezasha watu ,vikundi,taasisi na kampuni sawa na mahitaji yao kuwekeza pesa zao kwa meneja wa mfuko(UTT AMIS) kisha meneja huwekeza fedha hizo katika masoko ya fedha na masoko ya mitaji kulingana na waraka wa makubaliano. Faida ipatikanayo hugawanywa kwa wawekezaji kulingana na uwiano wa uwekezaji waliofanya katika mfuko husika.

MifukoyotehiiimewezakukidhivigezomuhimuvyauwekezajiambavyoniUsalama,UkwasinaFaida (Safety, Liquidity and Returns). 
Wawekezaji wote wananufaika kwakupata faida shindani hivyo kuweza kukuza mitaji yao, uwekezaji mseto hufanyika ili kupunguza hatariza uwekezaji, utalaamu wa meneja wamifuko, unafuu mkubwa wa gharama na uwazini vichocheo vinavyofanya UTT AMIS kuwa kimbilio lao.
UTT AMIS - Mshirika hakika katika uwekezaji.

 Bi. Surah Twaakyondo, Afisa kutoka UTT-AMIS akitoa maelezo ya jinsi ya kuwekeza kwenye Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja kwa wananchi waliotembelea banda wakati wa maonyesho ya NaneNane yaliyofanyika kitaifa mkoani Lindi.
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi akipata maelezo ya kina kuhusiana na mifuko ya uwekezajiwa pamoja inayoendeshwa na UTT AMIS. Kushoto ni Afisa Masoko na Uhusiano wa UTT AMIS Bw. Rahim Mwanga akitoa Maelezo hayo.
Waziri wa Fedha Dr.Philip Mpango (Kushoto) akisalimiana na Bw. Simon Migangala Kaimu Mkurugenzi mkuu  UTT AMIS  wakati alipotembelea banda la wizara ya fedha katika viwanja vya NaneNane Ngongo mkoani Lindi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad