HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 30, 2016

SEPTEMBA 16 KUZINDULIWA UPYA BENDI YA DAR MUSIC

Meneja wa Bendi ya Dar Music, Khamis Maero (Katikati)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutambulisha wasanii wapya wa bendi hiyo pia amesema kuwa wafanya uzinduzi wa Albamu yao Septemba 16 mwaka huu katika ukumbi wa Mango Gaeden Jijini Dar es salaam.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
BENDI ya Dar Music inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Septemba 16 huku uzinduzi huo ukisindikizwa na Malkia wa mipasho nchini Khadija Kopa pamoja na bendi ya Msondo.

Uzinduzi huo utaenda sambamba na utambulisho wa albamu ya bendi hiyo iliyobeba nyimbo 6 pamoja na video ya wimbo wao wa Chozi la Maskini.

Akizungumza na waandishi wa habari  Meneja wa bendi hiyo Khamis Maero amesema kuwa uzinduzi huo mkubwa unafanyika kwa mara ya kwanza toka Rais mpya Jado Fideforce aingie madarakani na kutambulisha wanamuziki wapya waliojinga na bendi hiyo.

Kwa upande wake Fide Force amesema kuwa nyimbo zitakazotambulishwa katika uzinduzi huo ni pamoja na wimbo uliobeba albamu yao ya Chozi la Maskini pamoja naSalmaga.

Nyimbo nyingine ni Bongo mchango, Maisha Upendo, Mtu Box, Jibebishe  na Ama zao Ama zangu.

"Ndani ya bendi yangu nimeamu kuchukua wanamuziki wazuri ili kuhimili ushindani uliopo katika tasnia ya muziki kutokana na ushindani uliopo" amesema Fideforce.

Fideforce kuwa ana uzoefu mkubwa na kile kinachopelekea bendi nyingi kuvunjika hivyo hawawezi kuruhusu kitu hicho kitokee ndani ya bendi yao.

"Uzuri ni kwamba ninaelewa muziki wa bongo ulivyo na nini huwa kinafanyika na kipi cha kuepuka ili bendi kutovunjika" , amesema Fideforce.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad