HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 3, 2016

NDEGE YA SHIRIKA LA EMIRATES YAPIGA MWELEKA DUBAI MCHANA WA LEO, HAKUNA ALIEPOTEZA MAISHA

Ndege ya abiria aina ya Boeing 777 mali ya Shirika la Emirates yenye namba EK521 iliyokuwa ikitokea Trivandrum nchini India, imepiga mweleka mchana wa leo katika Uwanja wa Ndege wa Dubai, ikidaiwa kugoma kwa gia ya kuruhu ndege kutua huku wengine wakisema ni kukosekana kwa mawasiliano katika Rubani na muongoza ndege wa Uwanja wa Kimataifa wa Dubai. Imeelezwa kuwa Abiria wote pamoja wahudumu waliokuwemo kwenye ndege hiyo walitoka salama kabisa isipokuwa Muhudumu mmoja tu ambaye alikimbizwa hospitali kwa uchunguzi zaidi. Ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria 282 pamoja na wasaidizi wa Ndege hiyo 18 ambao wote wako salama.
Muonekano wa uwanjani hapo baada ya Ndege hiyo kupiga mweleka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad