HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 27, 2016

WAKINA MAMA WA WILAYA YA KOROGWE WAFURAHIA MAFUNZO YA UJASILIAMALI YALIOFADHILIWA NA VODACOM TANZANIA FOUNDATION.

 Mwenyekiti wa kikundi cha 2Seeds kilichopo kijiji cha Tabora Korogwe Tanga,Asha Rajab akimuonyesha Meneja Ruzuku wa Vodacom  Tanzania Foundation, Sandra Oswald ( kushoto) moja ya mifuko yenye embe iliyotengenezwa kitalaam, tayari kwa kupelekwa sokoni, kwa mauzo. Kikundi hicho ni miongoni mwa vikundi Vinne  vilivyopata elimu ya ujasiriamali ,ufugaji,kilimo  kwa ufadhili wa Vodacom Tanzania Foundation  kwa  ushirikiano na shirika lisilo la Kiserikali la 2Seeds Network  la nchini Marekani  na kufanya kazi zake nchini.
 Meneja Ruzuku wa Vodacom  Tanzania Foundation Sandra Oswald(wapili kushoto) akipatiwa maelekezo na Mariam Jecha (wapili kulia)ambaye ni  bibi  masoko wa kikundi cha 2 Seeds  kilichopo kijiji cha  Tabora Wilaya ya Korogwe Tanga , juu ya utengenezaji na upakiaji wa viazi na mihogo vinavyozalishwa na kikundi hicho  baada ya kupata mafunzo  ya ujasiliamali toka taasisi isiyo ya kiserikali ya 2Seeds  ya nchini Marekani  yenye makazi yake makuu Wilayani humo, Mradi huo inafadhiliwa na Vodacom Tanzania Foundation,wengine kwenye picha ni wajumbe wakikundi hicho.
 Meneja Ruzuku wa Vodacom  Tanzania Foundation,Sandra Oswald (kulia) akishirikiana na wanakikundi cha 2Seeds, wa  kijiji cha  Tabora Wilaya ya Korogwe Tanga  kumenye viazi  kwa ajili ya kutengenza Clips  wakati alipotembelea kikundi hicho kukagua maendeleo ya miradi  mbalimbali ya ujasiliamali ,ufugaji, Kilimo iliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania Foundation kwa  kushirikiana na shirika lisilo la Kiserikali la 2Seeds Network  la nchini Marekani  na kufanya kazi zake nchini ambapo  makazi yake makuu  yapo Wilayani Korogwe.
 Mwenyekiti wa kikundi cha 2Seeds kilichopo kijiji cha Tabora Korogwe Tanga,Asha Rajab (Kulia)akimuonyesha Meneja Ruzuku wa Vodacom  Tanzania Foundation, Sandra Oswald ( kushoto) moja ya mashine ya jua inayotumika kukaushia  embe,na mbogamboga   iliyotengenezwa kitalaam,  wakati alipotembelea kikundi hicho kujionea maendeleo ya miradi mbalimbali ya ujasiriamali,Iliyofadhiliwa na Vodacom Tanzania Foundation  kwa  ushirikiano na shirika lisilo la Kiserikali la 2Seeds Network  la nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad