HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 17, 2016

WAENDESHA BODABODA WAFIKISHA FACEBOOK BURE KWA WATEJA WA AIRTEL SOKONI.

 Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwn Sunil Colaso akiwa na waendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda kabla ya kuingia sokoni kupeleka huduma ya facebook bure kwa wateja na watanzania kwa ujumla. Airtel wiki hii ilizindua huduma ya facebook bure inayowawezesha wateja wake kuunganishwa na ndugu jamaa na marafiki bure bila kuwa na haja ya kununua kifurushi chochote.
 Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwn Sunil Colaso akinyanyua bendera kuwaruhusu waendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda kuingia sokoni na kupeleka huduma ya facebook bure kwa wateja na watanzania kwa ujumla.
 Helikopta maalum ikiruka angani na kusambaza ujumbe wa huduma ya facebook bure kwa wateja wa Airtel na watanzania ili kuwawezesha kuwasiliana na ndugu jamaa na marafiki  na kuendesha shughuli za kijamii, uchumi kupitia huduma ya facebook bila gharama yeyote.
Baadhi ya waendesha pikipiki jijini  Dar es Salaam maarufu kama Bodaboda wakiondoka makao makuu ya Airtel kuingia  sokoni kupeleka huduma ya facebook bure kwa wateja na watanzania kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad