BAADA ya kumalizika kwa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara 2015/16 na Mbeya City fc kumaliza ikiwa kwenye nafasi ya 8 baada ya kuweka kibindoni jumla ya Pointi 35, kufuatia mabao 32 ya kufunga na kufungwa 34 kwenye michezo 30 ya msimu mzima.
Mlinzi Hassan Mwasapili (Kulia)ameweka rekodi ya kucheza mechi nyingi zaidi kikosini kuliko mchezaji yoyote kwa kucheza mechi 28 na kukosa 2 pia kuna rekodi kadhaa kutoka bechi la ufundi zimetoka na kati ya hizo baadhi zinaonyesha kuwa, magolikipa watatu wa kikosi cha kwanza, Juma Kaseja, Haningtony Kalyesubula na Geoffrey Mwalyego waliokuwa wakisimama langoni kwa kupishana kwenye michezo tofauti wamewajibika kwa asilimia 33.33 katika ushindi, sare na hata kupoteza mchezo katika mechi zote 30 za msimu.
Katika rekodi hizo zinaonyesha, Juma Kaseja amecheza michezo 17 na kuruhusu kufungwa mabao 20, Haningtony Kalyesubula akicheza michezo 13 na kufungwa mabao 14 wakati Geoffrey Mwalyego yeye hakupata nafasi ya kucheza mchezo hata mmoja.
No comments:
Post a Comment