HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 9, 2016

MAKALA YA SHERIA: SHERIA HAIKATAZI KUFUNGA NDOA IWAPO MMOJA WA WANANDOA HAYUPO

Na  Bashir  Yakub.

Mtu  mmoja  aliyeko  Zurich  alipiga  simu  akiuliza  swali  ambalo  ni  kichwa  cha  haya  makala .   Yeye  yuko  zurich  lakini  anataka  kufunga  ndoa  na  mwanamke  aliyeko  Tanzania  bila  kulazimika  kurudi  nchini. Anataka  afunge  ndoa  akiwa  hukohuko zurich  na  mwanamke  akiwa  Tanzania .

 Alisema  huko  aliko  jambo hilo linaruhusiwa  kisheria  ila  wasiwasi  wake  ni  kama  hata  Tanzania  jambo  hilo linaruhusiwa.  Kabla  ya  kutizama jambo  hilo  kisheria upo  umuhimu  pia wa  kutizama  baadhi  ya  mambo  kuhusu  ndoa.

1.NINI  MAANA  YA  NDOA.

Kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  9( 1 )  cha  sheria  ya  ndoa  sura  ya  29,  ndoa imetafsiriwa  kama  muungano  wa  hiari  kati  ya  mwanamke  na  mwanaume   wenye  lengo  la  kudumu  maisha  yao  yote. 

2.  SHERIA  INASEMAJE  KUHUSU WAZAZI   KUCHAGUA  WACHUMBA. 

Katika  maana  ya  ndoa  kuna  neno  hiari. Hili  ni  jambo  la  kwanza  katika  ndoa. Maana  yake  ni kuwa kusiwe  na  kulazimisha,  ulaghai,  udanganyifu n.k. Hata  kurubuni  kunakolenga  kuondoa  hiari  ya  mtu   nako  ni  kulazimishwa. Pia   wazazi  kuwachagulia  vijana  wao  wachumba  na  kuwashinikiza  kuwaoa  au  kuolewa  nao  nako  ni kuondoa  hiari  ya  wahusika.

 Si  kosa  mzazi  kuona mchumba  kwa ajili  ya kijana  wake isipokuwa  ni  kosa akitumia  nafasi hiyo   kulazimisha/kushinikiza  kufungwa  ndoa. Haya  ni  kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  16  cha  sheria  ya  ndoa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad