Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari juu ya uhamasishaji wa masuala ya Chakula Salama iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya waandis wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, hayupo pichani leo makao makuu ya TFDA jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula wa TFDA, Raymond Wigenge akizungumza na waandishi habari juu ya jamii kufuata taratibu za uandaji wa chakula ili kuweza kuwa salama kuepuka magonjwa yanayotokana viini vya vimelea vya magonjwa katika chakula iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
WANANCHI wametakiwa kuangalia usalama wa chakula ili kuweza kuepuka vimelea vya viini vya magonjwa yanayotokana na kula chakula kisicho salama.
Hayo ameyasema jana Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakulana Dawa (TFDA),Hiiti Sillo wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya uhamasishaji masuala ya usalama wa Chakula, amesema kula chakula chenye usalama inafanya kuwa taifa la maendeleo kiuchumi.
Amesema kuwa chakula ni muhimu kwa maisha ya binadamu kwa kula chakula ambacho hakijachafuliwa na viini vya magonjwa kama, kuhara,kipindupindu.
Sillo amesema watu milioni 91 duniani wanaugua magonjwa kutokana na kula chakula kilichochafuliwa na viini vya vimelea magonjwa.
Amesema TFDA licha kuwa na changamoto lakini wameweza kuwa na mafanikio kwa kuweka watendaji mipakani pamoja na viwanja vya ndege na bandari wa kufanya ukaguzi wavyakula vinavyoingia
Aidha amesema usalama chakula ni elimu endelevu hivyo kila mtu kwa nafasi yake ahakikishe anakula chakula salama ambacho hakina vimelea vinavyoweza kusababisha ugonjwa.
No comments:
Post a Comment