HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 9, 2015

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU (NBS) YASEMA PATO LA TAIFA LIMEONGEZA KWA ASILIMIA 7.9

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Morrice Oyuke akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya pato la Taifa kutokana na shughuli za Uchimbaji Madini, Mawe na Kokoto ziliongezeka kwa kasi ya asilimia 8.3 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 6.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2014. Kushoto ni Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa Daniel Masolwa.
Waandishi wa habari wakimsiliza Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke. (Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii). 

 OFISI ya Taifa ya Takwimu imesema pato la taifa limeongezeka kwa asilimia 7.9 huku sekta ya madini na uzalishaji umeme ikifanya kuongezeka kwa pato katika kipindi cha robo mwaka 2015 ikilinganishwa na kipindi cha mwaka 2014. Akizungumza Dar es Salaam leo asubuhi wakati wakati akitoa taarifa za pato la taifa robo ya pili ya mwaka kuanzia mwezi Aprili hadi Juni 2015, Mkerugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Morrice Oyuke alisema ongezeko hilo la takwimu ni la miezi mitatu ya mwaka huu.

 Oyuke alisema ongezeko hilo la pato la taifa linaenda sanjari na matokeo ya thamani ya pato la taifa kwa mwaka huu ambalo lilikuwa ni trilioni 89.0 ambapo katika robo ya mwaka ni trilioni 45.5 ikilinganishwa na trilioni 39.0 katika mwaka 2014.

 Alisema thamani ya pato la taifa ya robo mwaka ya trilioni 45.5 ni kubwa hivyo kusababisha pato la taifa la mwaka mzima linaweza kukuwa kama uchumi hautotetereka. "Kama uchumi hautaweza kuguswaguswa na matatizo mingene inaweza ikasababisha pato la taifa la mwaka huu likaongezeka badala ya ile iliyotegemewa hapo mwanzo,"alisema.

 Alisema ongezeko hilo la pato la taifa limechangiwa na sekta mbalimbali kufanya vizuri katika kipindi cha robo mwaka. Alisema sekta ambazo zimeongoza katika kipindi cha robo mwaka ni sekta ya madini,umeme,kilimo na mifugo,viwanda na ujenzi na huduma za kitaalamu.

 Alisema sekta ya uzalishaji umemere imekuwa kwa asilimia 18.5 huku bidhaa za viwandani ni asilimia 6.9 madini mawe na kokoto zimeongezeka asimilia 8.3 limeongezeka kutokana na shghuli za kiuchumi.

 "Kutokana na taarifa hii ya pato la taifa kwa robo mwaka taarifa hizi zitumike katika kupanga na kurekebisha sera mbalimbali za maendeleo ya nchi," alisema. Click here to Reply or Forward 1.75 GB (11%) of 15 GB used Manage Terms - Privacy Last account activity: 2 hours ago Details Cathbert Kajuna's profile photo Cathbert Kajuna Show details

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad