SHANGWE za muziki mnene wa 93.7 EFM ,kwa mara nyingine tena ziliendelea ndani ya bagamoyo . Burudani ya aina yake ikiongozwa na timu nzima ya EFM ilishushwa ndani ya mageti mia Adon lodge. Wakazi wa bagamoyo walipata nafasi ya kukutana na watangazaji, na RDJ’s huku wakifurahia burudani ya pamoja.
Muziki mnene bar kwa bar ulipambwa na kabumbu kati ya EFM na Bagamoyo veterani ambapo Bagamoyo veteran waliibuka na ushindi wa bao moja huku EFM wakiambulia sifuri.
Tangu kuanza kwa mechi hizi hii ni mara ya pili kwa 93.7 EFM kufungwa,mara ya kwanza ilifungwa bao mbili na buffalo fc ya kisarawe.
No comments:
Post a Comment