HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 12, 2015

WANAFUNZI 70 WA UHANDISI NA UDAKTARI KUONDOKA NCHINI SEPTEMBA 22, 2015 KWENDA KWA MASOMO NCHINI CHINA

Mkurugenzi wa Global Link Education (GEL) ambao ni Mawakala wa Vyuo Vya Nje ya nchi, Abdulmaliki Mollel akitoa maelezo katika semina ya kuwajengea uwezo wazazi na wanafunzi wanaokwenda kusoma Vyuo Vikuu vya China leo katika ofisi zao zilizopo viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wakilipia tisheti kwa ajili ya sare ya kutambuana wakati wa safari ya kwenda katika vyuo vya China katika semina ya kuwajengea uwezo wazazi na wanafunzi wanaokwenda kusoma Vyuo Vikuu vya China leo katika ofisi zao zilizopo viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Wanafunzi wakipata maelekekezo mbali mbali kutoka kwa Mkurugenzi wa Global Link Education (GEL) ambao ni Mawakala wa Vyuo Vya Nje ya nchi, Abdulmaliki Mollel katika semina ya kuwajengea uwezo wazazi na wanafunzi wanaokwenda kusoma Vyuo Vikuu vya China.
Mkurugenzi wa Global Link Education (GEL) ambao ni Mawakala wa Vyuo Vya Nje ya nchi, Abdulmaliki Mollel akibadilisha nawazo na wazazi walifika na watoto wao wanaotarajia kwenda kusoma vyuo vya China.
Wanafunzi wakiingia katika ofisi ya Global Education Link kupata maelezo mafunzo ya wanafaunzi wanaokwenda kusoma vyuo vya China. 
 
Wanafunzi wakiabadilishana mawazo mara baada ya kumaliza mafunzo yao leo, yaliyoendeshwa na GEL.
Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link,Abdulmalik Mollel akizungumza na wafanyakazi wake mara baada ya kumaliza mafunzo ya wanafunzi wanaokwenda kusoma nchini China.
 (Picha na Emanuel Massaka). 

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii Global Education Link (GEL) leo imeendesha mafunzo kwa wanafunzi wanaokwenda vyuo vya China kwa ajili ya kuanza safari na mazingira ambayo watayakuta katika vyuo hivyo. 

Akizungumza na katika mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wanafunzi 70 jinsi ya kuanza safari ya masomo katika vyuo vya China wanaotarajia kuondoka Septemba 22 mwaka huu, Mkurugenzi Mtendaji wa GEL, Abdulmaaliki Mollel amesema kuwa mafunzo hayo ni kuwaandaa wanafunzi jinsi ya kuanza safari yao kuanzia uwanja wa ndege hadi katika vyuo wanavyokwenda.

 Mollel aliwataka wazazi kuwa waangalifu na matumizi wanayopewa wakiwa vyuoni inapofikia inazidi inashawishi wanafunzi kufanya vitu visivyo na kuweza kufanya asiweze kupata elimu ambayo mzazi alikuwa anatarajia aipate huku nje.

 Katika Mafunzo hayo wanafunzi wamepewa nyaraka mbalimbali ambazo ni juu ya vyuo hivyo ambazo ni Chuo anachokwenda kuidhinishwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), Taarifa za nyaraka zenye alama za vidole kutoka katika jeshi la polisi kuonyesha wanafunzi hao hawana makosa ya kijinai. 

 Amesema kuwa Global Education Link imekuwa ikifanya kwa niaba ya vyuo vya nje ambavyo vina ubora wa kutoa elimu iliyobora ambayo itakuwa na tija kwa taifa pamoja na yeye mwenyewe. 

 Hata hivyo aliwataka wazazi kuwaandaa mapema watoto wao wanaokwenda kusoma ili kuweza kuondokana na usumbufu ambao unaweza kufanya asiweze kwenda huku akiwa ameshalipa ada pamoja na tiketi ya safari. Aidha Mkuirugenzi Mtendaji amesema kuwa utaratibu wote wa kuondoka na kufika katika vyuo hivyo anafanya ikiwa ni sehemu ya kuondokana na usumbufu kutokana na wanafunzi hao baadhi ni wageni katika kusafiri na ndege. 

 Mollel amesema wanaokwenda kusoma nchini China wengi wao ni masomo ya uhandisi wa Mafuta,Ndege,Ujenzi pamoja na udakitari kwa elimu juu waliomaliza kidato cha sita.

 Amesema nafasi katika masomo ya elimu juu bado zipo wanachotakiwa ni nkufanya mchakato wa mawasiliano wa kuweza kudailiwa hili ni moja ya makundi ambapo mengine yalishaondoka. 

Mollel amesema kuwa nafasi zipo katika vyuo vya nje kutokana kuendelea kufunguliwa kwa mawasiliano zaidi www.gel.co.tz na mawasilino ya simu ni+ 255 656 200 200. Aidha amewataka wazazi na wanafunzi kuacha kutumia baadhi ya watu walio katika nchi mbalimbali zenye vyuo kudai wao ndio wanajua ni uongo kwani Global Education Link ndio inaingia mikataba na vyuo vya nje na wengine hawajaingia mikataba.

 Kwa upande Mzazi Dk. Nicholas Eseko amsema mafunzo ni mazuri kwa kuwajengea uwezo wanafunzi wakti kuanza safari pamoja na mazingira watayoyakuta katika vyuo hivyo. 

Mwanafunzi Ismail Michael amesema kuwa mafunzo ni mazuri yanatoa mwanga wa kuanza safari ya kwenda katika vyuo hivyo vyenye ubora. “Sisi wanafunzi tunafarijika kwa kupata mwanga jinsi ya kuanza safari yetu na kujua vitu vibaya katika viwanja vya ndege ambavyo vinaweza ukafanya uwe uingie katika mikono ya dola”amesema Michael.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad