HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 17, 2015

PANONE FC KUFUNGUA DIMBA NA JKT OLJORO

Na Woinde Shizza,Arusha
TIMU ya panone FC ya mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro maarufu kama matajiri wa mafuta ,inatarajia kuanza kutupa karata yake ya mchezo wa kwanza wa ligi daraja la kwanza(FDL) dhidi ya maafande wa JKT Oljoro ya jijini Arusha.
Mchezo  huo utafanyika septemba 19 mwaka huu, katika uwanja wa Ushirika mjini moshi mkoani kilimanjaro,ambapo  baada ya mchezo huo pia wataikaribisha timu ya Polisi Tabora semptemba  26.
Katibu wa timu ya Panone FC  Augstino mwakatumbula alisema kuwa msimu  huu  wanaenda kuanza ligi daraja la kwanza  ambapo kila mchezo kwao ni fainali na watahakikisha wanatinga kucheza ligi kuu msimu wa 2016-2017.

“Tulifanya usajili mzuri wa wachezaji 7  ambao wameungana na wachezaji wetu tuliokuwa nao msimu uliopita na  tunaimani wataisaidia timu hii na tuna jumla ya wachezaji 27 wanaounda kikosi cha timu pia hatukuweza kuwasajili wote waliokuwepo hapo mwanzo na  ni kutokana na matatizo mbalimbali yakiwemo wengine  kutokuwa na nidhamu,uwezo wao umeshuka kimchezo.”alisema Mwakatumbula .


Aliwataja wachezaji hao saba  ambao wamefanikiwa kusajiliwa na matajiri hao wa mafuta kuwa ni pamoja na Ally Mseja ambaye ni mchezaji huru na Abdallah Shauri ‘Machopa’ aliyetokea timu ya Lipuli –Iringa wote wakiwa ni washambuliaji, Florence  Haure kutoka academy ya Kitayosce ya mkoani Kilimanjaro, Frank Kijoti aliyetokea AFC Arusha Rashid Gumbo kutoka  Kinondoni Manispaa ambaao wote ni Kiungo,Maulid Khalid kutoka  Singida United ambaye ni winga,Mansoul Mansoul  kutoka Coastal Union ya Tanga ambaye ni golikipa.

Timu hiyo ya Panone FC ipo kambini miezi miwili sasa ikijiweka tayari kwa ajili ya michuano hiyo ya ligi Daraja la kwanza ambapo inatarajiwa kucheza michezo ya kirafiki mapema wiki hii  na timu za  African sports,Magambo JKT na Coastal Union zote za Tanga .

Matajiri hao wa mafuta wananolewa na kocha Atuga  Manyundo akisaidiwa na msaidizi wake Azizi Nyoni .

Ligi daraja la kwanza ina shirikisha jumla ya timu 24 zilizogawanywa katika makundi matatu ambapo timu ya Panone ipo katika kundi ‘C’ na timu za JKT Olojro- Arusha,Polisi Mara –Mara,Rhino Rangers –Tabora,Mbao fc –Mwanza,Polisi Tabora  -Tabora,Geita Gold –

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad