HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 17, 2015

ARUSHA YAONGOZA MICHUANO YA WAZI TENISI KWA VIJANA.

 
Na Woinde Shizza,Arusha
Jiji la Arusha limeendelea kuwa kinara katika mchezo wa tenisi baada ya wachezaji wake kuibuka kidedea kwa kutwaa ushindi katika umri tofauti tofauti ,mashindano yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Arusha Tenisi gymkhana klabu.

Mashindano hayo yalidhaminiwa na Jubilee tyres ikiwa ni mwaka wa tatu sasa, yalishirikisha jumla ya wachezaji 90 ambao 28 kati yao ni wasichana kutoka Dar es salaam gymkhana klabu,Kijitonyama tenisi klabu kutoka Dar es salaam,Morogoro tenisi klabu, ISM –Moshi campus, AICC klabu –Arusha pamoja na Arusha tenis gymkhana klabu.

Katika umri wa miaka 6 kwa wasichana Schaefer Swantje kutoka ISM Moshi campus alifuatiwa na Suhana  Patel kutoka Arusha gymkhana klabu,huku kwa  upande wa wavulana wa umri huo Sahil Shah kutoka ISM moshi campus na kufuatiwa na Yuvraj Sidhu kutoka Arusha gymkhana klabu.

Wasichana walio na umri wa miaka 8 Asha Ali aliibuka mshindi na nafasi ya pili kumwendea Bahati Mdee wachezaji wote kutoka klabu ya AICC na kwa upande wa wavulana mika 8 Johnson Peter alibuka mshindi na kufuatiwa na Yasin Yusuph wote kutoka klabu ya AICC na kwa wasichana walio na umri wa miaka 10 Vanessa Emmanuel kutoka AICC aliibuka kidedea na kufuatiwa na Caroline Mwangata wa ISM Moshi campus, huku kwa wavulana miaka hiyo Rashid Abdallah kutoka Arusha gymkhana klabu na kufuatiwa na Abdumarik Kudra kutoka Morogoro klabu.

Kwa umri wa miaka  12 wasichana Shana Martin aliongoza na kufuatiwa na  Fei Amon wote kutoka Arusha gymkhana klabu na wavulana Damas Felex na nafasi ya pili kumwendea Benjamini Laurance wote kutoka AICC ,Huku kwa umri wa miaka 14 kwa wasichana Jackline Kayuga kutoka kijitonyama Tenisi klabu na nafsi ya pili Anikaa Aggarwal  kutoka Arusha Gymkhana klabu na kwa wavulana wa umri huo Deogratius Felex  na kufuatiwa na Yusufu Laurance wote kutoka AICC.

Jackline Kayuga kutoka  Kijitonyama Tennis klabu alishika nafasi ya kwanzana kufuatiwa Hawa Yahya kutoka Dar es salaam gymkhana klabu katika umri wa miaka 16 kwa  wasichana  na kwa  wavulana Omari Sulle Arusha Gymkhana klabu na kufuatiwa na Hassan Hamisi - AICC Club Arusha.

Kwa upande wa umri wa miaka 18 kwa wasichana hawakuwepo ,na walicheza wavulana pekee ambapo Emmanuel Mallya- Arusha Gymkhana Club alifuatiwa na -  Frank Menard -Arusha Gymkhana Club.

Nicholaus Leringa Kocha mkuu  wa klabu ya AGC alisema kuwa  mashindano hayo hufanyika kila mwaka yakiwa na lengo  la kuwaimarisha vijana katika dhana nzima ya  kunyanyua vipaji vyao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad