HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 31, 2015

UFAFANUZI WA JESHI LA POLISI JUU YA TUKIO LA KULA NJAMA NA KUJARIBU KUMTOROSHA ASKOFU JOSEPHAT GWAJIMA AKIWA HOSPITALI

Leo tarehe 30/03/2015 waandishi wa habari walifika kituo Kikuu cha Polisi wakitaka kujua uhalali wa silaha iliyokamatwa tarehe 29/03/2015. Silaha hiyo ni Bastola aina ya BERRETA yenye namba CAT5802 ikiwa na risasi tatu. Pia zilikamatwa risasi 17 za Short Gun.

Ufafanuzu ni kama ifuatavyo:

Uchunguzi wa kina na wa kitaalam sasa umethibitisha kwamba silaha hiyo inamilikiwa kihalali na Askofu Josephat Gwajima. Kuhusu risasi 17 za Short Gun ni kwamba Askofu Gwajima anamiliki Bunduki aina ya Short Gun yenye namba 102837 ambayo inatumia risasi za aina ya hizo zilizokamatwa.

Kuhusu watu 15 wanaotuhumiwa kujaribu kumtorosha Askofu Josephat Gwajima bado uchunguzi unaendelea. Aidha watu hao pia wanahojiwa kuhusu suala la kukutwa na silaha na risasi zilizotajwa hapo juu wakati wao sio wamiliki halali za silaha hiyo na risasi hizo na idadi iliyotajwa kwa mujibu wa sheria.

Baada ya uchunguzi wa suala hilo jalada la kesi litapelekwa kwa mwanasheria wa Serikali kabla hawajafikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.

KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM,
S. H. KOVA,
DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad