Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umenyakua tuzo tatu za ubunifu
katika sekta ya hifadhi ya Jamii Barani Afrika zinazosimamiwa na
Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Duniani (ISSA).
Halfa ya kukabidhi tuzo hizo ilifanyika Jijini Casablanca nchini
Morocco usiku wa tarehe 3 Desemba, 2014 katika hoteli ya Serana jijini
Casablanca ambapo washiriki zaidi ya 360 kutoka taasisi 75 katika
mataifa 45 ya Afrika zilihudhuria.
Tuzo ambazo NHIF ilikabidhiwa ni katika eneo la utoaji wa huduma za
matibabu za kibingwa maeneo magumu kufika, kazi ambayo mfuko umefanya
kwa kushirikiana na wataalamu wa hospitali za rufaa nchini. tuzo
nyingine ni katika eneo la TEHAMA katika utayarishaji madai na huduma
za matibabu kwa wanachama wastaafu.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo wa Kanda ya Afrika ambacho pia
kilijadili mambo muhimu kuhusu sekta ya hifahi ya jamii na kutambua
kazi za ubunifu uliongozwa na Waziri wa kazi Mheshimiwa Gaudensia
Kabaka pamoja na Viongozi waandamizi wa Mamlaka ya Usimamizi na
Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini (SSRA) na baadhi ya
Watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini.
Tangu kuanza kutolewa kwa ambazo hushindaniwa kila baada ya miaka
mitatu, NHIF imeng'ara mara zote.Mwaka 2008 ilipata tuzo ya cheti cha
heshima cha ubunifu mjini Kigali kwa kuwashirikisha wadau wake katika
utoaji wa elimu kwa makundi mbalimbali ngazi ya mkoa. Mwaka 2011
ulikuwa mshindi wa kwanza wa jumla barani Afrika na mwaka huu umeibuka
tena na ushindi huo muhimu unaoitangaza Tanzania kimataifa kupitia
Bima ya Afya.
Mbali ya NHIF, Tanzania pia imengara kwa kuzoa jumla ya tuzo 6 mbapo
Mamlaka ya Udhibiti ya SSRA, Mfuko wa Pensheni wa PPF na Mfuko wa PSPS
pia ilijizolea tuzo moja moja kwa kila mmoja hivyo kufanya Tanzania
kuwa na jumla ya tuzo 6 na kuifanya kuwa kinara katika ukanda wa nchi
za Afrika mashariki na ya Kati.
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii katika nchi nne ilipata heshima ya pekee
kwa kazi zao za ubunifu. Mifuko hiyo ni kutoka Cameroon yenyewe
iliyonyakua tuzo 8, Gabon, Maurtania, wenyeji Morocco.
Washindi wa jumla wa kwa mwaka 2014 ni wenyeji Morocco na Jirani zao
wa Mauritania ambao kwa pamoja wamepata tuzo ya jumla kwa kutoa huduma
bora, kuongeza uwigo wa wanaonufaika na huduma za mifuko hiyo hasa
wasio na uwezo, matumizi ya TEHAMA na huduma kwa wateja na ufanisi kwa
ujumla.
Baadhi ya Washindi wa Tuzo zitolewazo na Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Duniani (ISSA) wakifuatilia sherehe hiyo iliyofanyika katika hotel ya Sheraton Mjini Casablanca. SSRA pia ilishinda tuzo 1 ya ubunifu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Bw Hamis Mdee akiwasilisha mada kuhusu huduma za matibabu za kibingwa zinazoratibiwa na NHIF maeneo ya vijini kwa kushirikiana na hospitali za rufaa.
Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Hamis Mdee (wa pili kulia) akikabidhiwa Tuzo za Ubunifu ambazo NHIF ilinyakuwa tuzo 3 Barani Afrika Mjini Casablanca Mwishoni mwa Juma.
Kundi moja la watoa mada katika moja ya session za kuelezea kazi za ubunifu zilizofanywa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Barani Afrika.
Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Gaudensia Kabaka na Mwenyekiti wa SSRA,Bw Juma Muhimbi na Bw Mwanjali kutoka Wizara ya Kazi wakiwa katika picha ya pamoja na timu ya NHIF.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Hamis Mdee akipongezwa na Rais wa ISSA Bw Errol Frank kulia na Makamu wake Bw Said Ahmidouch wanaomsaidia kubeba tuzo hizo za cheti cha heshima cha ubunifu.
Jiji la Casablanca na pilika pilika zake wakati wa mchana Siku za Ijumaa hakuna pilika pilika nyingi.
No comments:
Post a Comment