HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, September 14, 2014

WASHINDI TUZO ZA HABARI ZA TANAPA 2013 WAENDELEA KUTEMBELEA MAENEO MUHIMU YA UTALII NA HISTORIA AFRIKA KUSINI

 Mwanahabari Vedasto Msungu wa ITV (kushoto) na David Rwenyagira (Radio 5) walikuwa miongoni mwa wanahabari waliofika nje ya Jengo la Mahakama Kuu ya Pretoria ambapo ilikuwa siku muhimu ya utoaji hukumu kwa mwanariadha Oscar Pistorius aliyeshitakiwa kwa makosa ya kumuua mpenzi wake kwa silaha. Unayoyaona hapo nyuma ni magari maalum ya urushaji tukio hilo moja kwa moja katika vyombo mbalimbali vya habari duniani(OB Van) na mahema meupe ni Kambi iliyopigwa na wanahabari hao kwa ajili ya kufuatilia tukio hilo muhimu.
Wanahabari Vedasto Msungu na David Rwenyagira walipata nafasi ya kumhoji raia huyu wa Afrika Kusini juu ya maoni yake kwa hukumu iliyotarajiwa kutolewa.
 Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 waliweza kufika hadi katika Hifadhi ya Taifa ya Pilanesberg ili kujionea wanyama mbalimbali. Kutoka Kushoto ni Mtanzania Peter Masika anayeishi Johannesburg, Vedasto Msungu (ITV), Pascal Shelutete(Meneja Mawasiliano TANAPA) na Gerald Kitabu wa The Guardian.
 Wanyama aina ya Nyumbu wanaopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Pilanesberg.
 Washindi wa Tuzo za TANAPA 2013 waliweza pia kufika katika Mji wa Sun City kama wanavyoonekana hapa.
 Washindi wa Tuzo za TANAPA 2013 waliweza kupiga picha na watalii mbalimbali katika jiji la Sun City.
 Washindi wa Tuzo za TANAPA 2013 walikuwa kazini pia kama Vedasto Msungu (kulia) wa ITV hapa anaonekana akimhoji Mtanzania Peter Masika (kushoto).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad