HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 31, 2014

Mh. Pinda Mgeni Rasmi Mtwara Festival 2014

Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda akiwa katika picha na Bw. Anic Kashasha, Mwenyekiti Mtendaji wa TACIN alipomtembelea  nyumbani kwake Oyserbay, Dar es Salaam, jana Jumapili, tarehe 30 Julai, 2014 kumpa taarifa ya maendeleo ya maandalizi ya Mtwara Festival, itakayofanyika tarehe 16 - 17 Agosti, 2014 katika viwanja vya Chuo Cha Ualimu Mtwara(TTC). Mh. Mizengo Pinda, atakuwa Mgeni Rasmi wa Mtwara Festival, ambao ni mpango mkakati wa mawasiliano wa kuhamasisha wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi, kizitambua fursa shirikishi zinazosisimuliwa na uchumi wa gesi asilia. Kauli mbiu ya Mtwara Festival ni "FURSA ZIMEFUNGUKA, TUZITAMBUE, TUJIANDAE, TUZICHANGAMKIE". Akizungumza mara baada ya kukutana na Waziri Mkuu, Bw. Kashasha alisema mpango huo wa elimu kwa umma, utachangia kwa kiasi kikubwa kutengeneza ajira na kipato kwa wananchi wa mikoa hiyo na hivyo kubadilisha hali za maisha ya wananchi hao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad