HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 2, 2014

Waziri Lukuvi akutana na waandishi wa habari jijini Dar leo kuzungumzia ratiba ya mazishi ya Marehemu Dr. William Mgimwa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mhe.William Lukuvi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Mazishi ya aliyekuwa waziri wa Fedha Marehemu Dk. William Mgimwa akiongea na waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu mwili wa marehemu kuwasili tarehe nne saa saba mchana uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere na Shirika la Ndege la Afrika ya Kusini na kuzikwa tarehe sita katika kijiji cha Magunga mkoani Iringa. Kulia ni Naibu waziri wa Fedha Saada Salum Mkuya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mhe.William Lukuvi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Mazishi ya aliyekuwa waziri wa Fedha Marehemu Dk. William Mgimwa akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) ratiba ya mazishi ya Marehemu Mgimwa aliyefariki jana nchini Afrika ya Kusini alikokuwa anapata matibabu. Kulia ni Naibu waziri wa Fedha Saada Salum Mkuya.
Katibu Mkuu ofisi ya Waziri Mkuu Dk. Florens Turuka (kulia) na Katibu Mkuu wizara ya Afya na Stawi wa Jamii Charles Pallangyo (kushoto) wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mhe.William Lukuvi (hayupo pichani) wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu ratiba ya mazishi ya aliyekuwa waziri wa Fedha Marehemu Dk. William Mgimwa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mhe.William Lukuvi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Mazishi ya aliyekuwa waziri wa Fedha Marehemu Dk. William Mgimwa akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu ratiba ya mazishi ya Marehemu Mgimwa ambapo mwili wa marehemu utawasili tarehe nne saa saba, ibada na heshima za mwisho zitatolewa tarehe tano katika ukumbi wa Karimjee na mazishi yatafanyika tarehe sita katika kijiji cha Magunga mkoani Iringa.
Wapigapicha kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakimpiga picha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mhe.William Lukuvi (hayupo pichani) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Mazishi ya aliyekuwa waziri wa Fedha Marehemu Dk. William Mgimwa wakati akiongea nao leo jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano uliopo Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu ratiba ya mazishi. Picha na Anna Nkinda - Maelezo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad