HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 30, 2013

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AZINDUA TOVUTI KUU YA SERIKALI

Waziri Mkuu Mizengo Pinda (katikati) akiwa ameambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Celina Kombani wakiwasili katika Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao kupata maelezo ya Tovuti Kuu ya Serikali kabla ya kuizindua tovuti hiyo leo jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tovuti Kuu ya Serikali www.tanzania.go.tz itakayowawezesha wananchi kupata taarifa na huduma mbalimbali za serikali kwa urahisi, haraka na kwa wakati. Wanaoshuhudia kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Celina Kombani na Dkt. Jabiri Bakari ,Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao ambao ni wasimamizi wa Tovuti hiyo.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akifurahia jambo mara baada ya kuzindua Tovuti Kuu ya Serikali na kuwataka wananchi kuitumia katika kupata taarifa mbalimbali za serikali.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipata maelezo kuhusu uundwaji wa Tovuti Kuu ya Serikali na namna inavyoendeshwa kutoka kwa Mkurugenzi wa Msaidizi wa Mifumo Shirikishi ya Umma Bw. Fratern Hassani (kulia) katika Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao wasimamizi wa Tovuti Kuu ya Serikali. Wengine wanaosikiliza kutoka kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Wakala hiyo Dkt. Jabiri Bakari, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Celina Kombani,Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa, Makatibu wakuu na watendaji wengine wa serikali.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza jambo mara baada ya kupata maelezo kuhusu mifumo ya uendeshaji wa Tovuti Kuu ya Serikali alipokutana na wataalam wanaosimamia Tovuti hiyo katika Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao jijini Dar es saalam. Picha na 6. Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakitekeleza makumu yao wakati wa uzinduzi wa Tovuti Kuu ya serikali katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Dkt. Jabiri Bakari akitoa ufafanuzi kwa wadau mbalimbali juu ya wa namna Tovuti Kuu ya Serikali inavyofanya kazi na namna ya kupata taarifa za serikali wakati wa uzinduzi wa Tovuti hiyo jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi wa Wakala ya Serikali Mtandao waliofanikisha uzinduzi wa Tovuti Kuu ya serikali.
Baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ambayo ndiyo msimamizi wa maudhui ya Tovuti Kuu ya Serikali kupitia Idara ya Habari –MAELEZO waliohudhuria Uzinduzi wa Tovuti Kuu hiyo.Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Bw. Raphael Hokororo akifuatiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene.
Waandishi wa habari wakiwajibika. Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad