Habari wadau Wangu wote,
Naomba kuwathibitishia kuwa mimi Kala Jeremiah Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,page yangu ya Facebook imeibiwa na matapeli wa kwenye mitandao na wameshaanza kuitumia na wameanza kwa kutoa tangazo la mikopo.
kwa hiyo nawataarifu kwamba anaefanya hivyo,siyo mimi ni matapeli. Inauma sana kuona nimehangaikia page hii mpaka hapo ilipofikia ina like zaidi ya 52, 000 watu zaidi ya elfu hamsini na mbili.
Nimeamua kuanzisha page mpya ndo naishughulikia sasa inaitwa KALA 0444 (BOFYA HAPA KUIONA) poleni sana kwa usumbufu.
Nni mimi rafiki yenu Kala Jeremiah


No comments:
Post a Comment