HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 26, 2013

Waziri Mkuu Mizengo Pinda awasili Mkoani Tanga

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Mizengo Pinda akiwasili katika uwanja wa ndege wa Mkoa wa Tanga kwa ajili ya Kongano la Uwekezaji Kanda ya Kaskazini litakalofanyika Septemba 26-27 mwaka huu. Mara baada ya Mapokezi Mhe. Pinda atapokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Tanga katika ukumbi wa mikutano wa Tanga Beach resort.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Mizengo akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Bw. Benedict Ole Kuyan. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Chiku Gallawa.
Mhe. Pinda akisalimiana na Viongozi wa ngazi za juu katika Mkoa wa Tanga.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Mizengo akifurahia burudani ya vikundi mbalimbali vya ngoma ( havipo pichani) mara tu baada ya kuwasili katika Mkoa wa Tanga. ( wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Halima Dendego na kulia kwake ni Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda.
Burudani mbalimbali. Picha zote na Monica Laurent, Afisa Habari Mkoa wa Tanga.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad