HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 27, 2013

NATHAN MPANGALA, MARAFIKI WA WAFANYE WATABASAMU WACHORA PAMOJA NA WATOTO HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

Mratibu wa mradi wa kujitolea wa Wafanye Watabasamu, Katunisti Nathan Mpangala ‘Mtukwao’, akishea jambo na mmoja wa malaika Hospitali ya Taifa Muhimbili, upande wa saratani, Jumammosi iliyopita.
Mmoja wa watoto wanaendelea na matibabu Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, akiwa bize na rangi wakati walipotembelewa na mchora katuni Nathan Mpangala kupitia mradi wake wa kujitolea wa Wafanye Watabasamu, Jumamosi iliyopita. Mradi huo unaoshirikisha ndugu, jamaa, marafiki na wachoraji wenzake, ulikwenda kuwafariji kwa kuwapa zawadi kisha kuchora nao.
Marafiki wa Wafanye Watabasamu, walionesha tabasamu mapemaaaaa.
Sanaa inamchango mkubwa katika kupunguza msongo wa mawazo na kusahaulisha maumivu.
Mchora vibonzo wa ITV ambaye pia ni mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala akiwa na mchora vibonzo wa baadae.
NYUMBA TU, SIMPO. Akiendelezwa atakuja kuwa mchoraji mahiri wa majengo.
Mchoraji katuni wa gazeti la Nipashe, Abdul King O aka ‘Kaboka mchizi’, aliungana na Wafanye Watabasamu kuwatabasamisha malaika hawa. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad