HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, August 10, 2013

Jimmy Master kutoka na Double J Final mapema mwezi ujao

YULE mkali wa Muvi za kibongo na muongozaji wa muvi hizo,Jimmy Mponda a.k.a  'Jimmy Master' aliyewahi kutikisa na mfululizo wa filamu za misuko iliyotoka sehemu ya kwanza hadi ya tatu na Sasa amekuja na kitu kingine kipya kabisa kiitwacho Double J Final ambayo itazinduliwa rasmi hivi karibuni,huku ukiwa ni ujio wa mwisho kutoka baada ya kutangulia na Doble J sehemu ya kwanza na yapili zilizotoka mwaka jana.

"Mwaka jana nilifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa filamu hususani wanaopagawa na filamu za mapigano na kujawa mambo ya kipelelezi,"alisema J Plus.

Alisema Doble J Final pia ni ujio wake wa filamu nyingine ya mapigano na kuna heka heka za kipelelezi ndani. J Plus aliyezoeleka sasa katika kuonesha ubabe wa kufa mtu , kwa sasa ujio wake huo unatazamiwa kuingia sokoni mapema tu , mwezi ujao .

Pia Jimmy Master amemshirikisha mbabe mwingine katika filamu za mapigano Ibrahim Mbwana 'Bad Boy' na pia wamo nyota wengine katika dulu la filamu kama Charles Magari , Hashim Kambi na Veronica Viankero.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad