Taswira ya Ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ulivyokuwa siku ya Alhamisi wakati wa mkutano uliojadili hali katika eneo la Maziwa Makuu, mkutano huo ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon, Mwakilishi wake wa Maziwa Makuu Mary Robinson, Mawaziri kutoka nchi za Maziwa Makuu, SADC , Umoja wa Afrika, EU, na Mkuu wa Banki ya Dunia aliyeongea kwa njia ya Video kutokea Makao Makuu ya Banki hiyo jijini Washington.
Mwakilishi
wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi
akizungumza kwaniaba ya Serikali katika mkutano huo ambapo alilitaka
Baraza Kuu la Usalama Kudai ushahidi dhidi ya tuhuma na propaganda za
uongo ambazo zimekuwa zikielekezwa dhidi ya Uongozi wa Juu wa Brigedi
Maalum ambayo inaundwa na wanajeshi kutoka Tanzania, Afrika Kusini na
Malawi. Akasema tuhuma hizo zinazoipaka matope FIB bila ya sababu
zote za msingi zinalenga katika kudhoofisha mamlaka ya Brigedi hiyo na
MONUSCO kwa Ujumla katika kutafuta amani ya kudumu DRC na kwamba
Baraza Kuu linawajibu wa kuwalinda wale wote ambao siyo tu wamejitolea
kusaidia upatikanaji wa amani lakini pia wanabeba dhamana iliyoadhimu.
Tanzania ilikuwa kati ya nchi chache zilizoalikwa kuzungumza katika
mkutano huo.
Waziri
wa Mambo ya Nje wa Marekani, Bw. John Kerry, alizungumza wakati wa
mkutano wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, uliokuwa
ukijadili hali katika eneo la Maziwa Makuu na uungaji mkono Mpango
Mpana wa Kisiasa wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano
wa Maendeleo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Maziwa Makuu.
Mkutano huo uliokuwa katika ngazi ya Mawaziri umeandaliwa na Marekani
ambaye ni Rais wa Baraza hilo kwa mwezi huu wa Julai. katika hotuba
yake, Waziri Kerry amesema Marekani inakaribisha na kuunga mkono
upelekaji wa Brigedi Maalum ( FIB) katika eneo la Mashariki ya Kongo na
pia inaunga mkono na itashirikiana na nchi 11 zilizotia saini
Mpango mpana wa kisiasa ili kuhakikisha unatekelezwa na
kufanikiwa.
No comments:
Post a Comment