HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 22, 2013

PPF yatoa msaada wa madawati kwa shule za msingi Mtwara

Kaimu Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Mtwara,Bi. Kauthar Nassoro (kushoto) akipeana mkono na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Mtwara,Bw. Ally Mpenye wakati wa zoezi la kukabidhi sehemu ya msaada wa madawati 30 yenye thamani ya Tshs milioni mbili na laki saba yaliyotolewa na Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.
Kaimu Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Mtwara,Bi. Kauthar Nassoro akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanyika kwa makabidhiano hayo,ambapo alieleza umuhimu wa fao la elimu ambalo linatolewa na Mfuko wa Pensheni wa PPF pekee.
Baadhi ya Maofisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Mtwara wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukabidhi msaada wa madawati.kutoka kulia ni Kauthar Nassoro,Tumpe Mwaitenda,Lilian Mhina pamoja na Shida Michael.
Viongozi wa halmashauri ya Mtwara,Kaimu Mkurugenzi Bw.Ally Mpenye na Kaimu afisa elimu wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad