HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, April 23, 2013

Vodacom yazidi kuboresha mazingira ya shule za msingi vijijini

 Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim (katikati) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule (kulia) na Katibu wa Mbunge wa Songwe Agapito Kilongozi kabla ya kuanza kwa hafla ya makabidhiano ya vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi Mkwajuni Wilayani Chunya mwishoni mwa wiki.
 Katibu Tawala Wilaya ya Chunya Sosthenes Mayoka akikabidhi funguo za vyumba vitatu vya madarasa kwa Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Mkwajuni Wilayani Chunya baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa na Vodacom Foundation. Anaeshuhudia ni Mkuu wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule. Hafla hiyo imefanyika mwishoni mwa wiki.
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mkwajuni Wilayani Chunya Mkoa wa Mbeya wakifuatilia kwa furaha hafla ya makabidhiano ya vyumba vitatu vya madarasa vilivyofanyiwa ukarabati mkubwa na Vodacom Foundation katika mikakati yake ya kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu nchini. Hafla hiyo ilifanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki iliyoongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Chunya Sosthenes Mayoka.
 Wanafunzi wakifurahia madarasa mapya
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim akiwa na wanafunzi wa darasa la sita wa shule ya msingi Mkwajuni Wilayani Chunya Jackson Anthon (kulia) na mwenzake Erica Agustino. Wanafunzi hao walijibu kwa ufasaha maswali ya ufahamu wa huduma za Vodacom ya Cheka nao na M-pesa wakati wa hafla ya makabidhinao ya vyumba vitatu vya madarasa vilivyokarabitiwa na Vodacom Foundation. Vodacom Foundation imeahidi kuwapatia wanafunzi hao vifaa vya shule, sare na vitabu vya kiada kwa ajili ya darasa la sita na la saba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad