Mkuu wa Kiengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma akizungumza wakati wa Warsha ya siku tatu kwa wamiliki na waendeshaji wa mitandao ya Kijamii (BLOGS) hapa nchini kuhusu Wizara hiyo inavyoweza kupeleka habari kwa urahisi kwa wananchi wa kawaida iliyofanyia Kibaha mkoani Pwan,hivi karibuni.
Baadhi ya wamiliki na waendeshaji wa mitandao ya kijamii (Blogs) wakimsikiliza Mkuu wa Kiengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma (hayupo pichani) wakati wa warsha hiyo ya siku tatu
Baadhi ya wamiliki na waendeshaji wa mitandao ya kijamii (Blogs) waliohudhulia Semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Na Othman Michuzi, Mtaa kwa Mtaa Blog
Kutokuwa na utamaduni wa Watanzania walio wengi kupenda kusoma vitabu, na taarifa mbali mbali
zinazohusiana na maendeleo ya nchi imetajwa kuwa ni kikwazo kikubwa
katika mawasiliano kati ya wananchi na taasisi mbali mbali za serikali,
jambo ambalo ni hatari katika Taifa linaloendelea.
Kwa mujibu wa utafiti usio rasmi uliofanywa na baadhi ya waandishi wa
habri za kijamii nchini, ni asilimia tisa tu ya watanzania, ndio wenye
utaratibu wa kupenda kusoma, asilimia iliyobakia, hupata habari kwa njia
ya kusikia, ama kwenye vyombo vya habari au kwenye maongezi ya kawaida.
Hii ni moja ya taarifa zilizowasilishwa kwenye warsha ya siku tatu
iliyoshirikisha baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii na magazeti tando, kwa
kushirikiana na Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Fedha, katika
kujadili jinsi ya kuboresha mawasiliano kati ya wananchi na taasisi za
kimaendeleo ili kurahisisha ufikaji wa taarifa za kimaendeleo kwa
wananchi.
Kutokana na tabia hii ya kutopenda kusoma, wananchi wengi wamekuwa
wakikosa kujua mambo mengi ya kimaendeleo yanayofanyika nchini kwa
sababu taarifa hizi mara nyingi huwekwa katika maandishi.
"Limekuwa ni tatizo kubwa sana hapa nchini, watu hawajui kitu na hawataki
kujua kwa sababu hawapendi kusoma", alisema wakati akichangia mada mmoja
wa washiriki wa Warsha hiyo,Bw. Josephat Lukaza.
Katika Warsha hiyo ya siku ambayo pia ilihudhuriwa na maafisa habari
kutoka sekta mbali mbali za kimaendeleo, wadau walikuwa wakitafuta njia
mbadala itakayosababisha wananchi kujua mambo mbalimbali ya kimaendeleo
ya nchi ili kujua hali halisi ya uchumi wa nchi inavyoendelea.
Naye Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha Wizara ya fedha, Bi Ingiahedi
Mduma, alisema ipo haja ya kuwa wabuhifu katika kuhakikisha kwamba kwa
njia yoyote ile, tunahakikisha kwamba wananchi wa kawaida, hasa wa
vijijini, wanapata taarifa husika kwa wakati muafaka.
Amesema taarifa za kimaendeleo za nchi ni haki ya kila mwananchi kujua
na ndio maana sasa wameamua kukaa chini na kuumiza vichwa katika kutaka
kujua jinsi ya kuwafikia asilimia kubwa ya wananchi, mijini na vijijini.
Warsha hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Kilimanjaro Park Hotel, maeneo
ya Misugusugu, wilayani Kibaha, mkoa wa Pwani ambapo pia mikakati mbali
mbali ya kimaendeleo ilijadiliwa.
No comments:
Post a Comment