HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, January 5, 2013

WENGI WAJIUNGA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII KIMANZICHANA.

Wakazi wa Kijiji cha Kimazichana Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani wakijiandikisha Uwanachama kwenye Mfuko wa Afya ya Jamii mara baada ya uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga kwenye mfuko wa Afya ya Jamii leo kijijini hapo. Hadi mtandao huu unatoka eneo la tukio zoezi hilo lilikuwa likiendelea. Kaya miasaba tu ndizo zimejiunga na mfuko huo kati ya kaya Hamsini na moja elfu zilizopo kwenye wilaya hiyo.
Tunajiunga na mfuko! Baada ya kueleweshwa faida za kujiunga na mfuko huo walikusanyika kwa mwandishi na kuanza kujiunga.
Mratibu wa mpango huo kutoka CHF Rehani Athumani (kushoto) akizungumza na wananchi wa Kimanzichana Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo, wapili kulia ni Mbunge wa jimbo la Mkuranga Adam Malima.
Mbunge wa Mkuranga Adam Malima akiwahutubia wakazi wa kijiji Cha Kimanzichana wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji huo wa mfuko wa afya ya jamii, kulia ni mwakilishi wa Katibu Tawala wa Halmashauri ya Mkuranga Dismas Makandawa na Kaimu Mkuu wa Wilaya hiyo Ally Fadhili Msuya.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi huo leo.
Awali Mbunge huyo wa Mkuranga akisalimia viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga pamoja na wa  Mfuko wa Afya ya jamii.
Mbunge wa Mkuranga Mh.Adam Malima, akimkabidhi kadi ya uwanachama wa mfuko wa afya ya jamii Mzee Saleh Salum Kihedu mara baada ya kujiunga rasmi.

WAKAZI wa Kijiji cha Kimanzichana Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani wamejitokeza kwa wingi kujiunga kwenye mfuko wa  afya ya jamii wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na mfuko huo unaosimamiwa na taasisi ya NHIF uliofanyika leo.
Timu ya kampeni ya uhamasishaji wa kujiunga na mfuko huo ikiongozwa na mratibu wa CHF Rehani Athumani, itakuwepo wilayani humo kwa kufanya uhamasishaji huo kwa njia mbalimbali zikiwemo za sinema na mikutano ya hadhara, hadi mtandao huu unaondoka eneo la tukio zoezi hilo lilikuwa likiendelea kwenye Kijiji hicho.
Mfuko wa afya ya jamii unaziwezesha kaya husika kwenye halmashauri kupata matibabu kwenye hospitali za serikali kwenye Wilaya husika kwa gharama ya Shilingi elfu tano kwa mwaka mzima huku kiwango cha ukubwa wa familia ni Mkuu wa kaya na watoto watano wasiozidi umri wa miaka 18.
Wananchi wengi kwenye jimbo hilo hawajajiunga kwenye mfuko huo, kutokana na taarifa iliyosomwa kwenye mkutano ni kaya miasaba ( 700) tu kati ya kaya Hamsini na moja elfu (51,000) zilizopo kwenye jimbo hilo. 
Aidha kwenye uzindduzi huo ambao mgeni rasmi alikuwa Mbunge wa jimbo la Mkuranga Kigoma Malima wananchi waliuliza maswali mbalimbali kwa mbunge wao huku wakiwa na maswali mengi yaliyokuwa nnje ya malengo ya mkutano huo ambayo hata hivyo mbunge huyo aliruhusu yaulizwe.
Akijibu baadhi ya maswali mbunge huyo aliwataka wananchi hao kutopuuza fursa hizo ambazo ni za msingi huku wakizingatia zaidi kwamba umuhimu huo upo zaidi kwa watoto na kina mama kwani ndio huteseka zaidi kwenye suala la huduma za afya.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad