Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nchi, Mwamini Malemi akimkaribisha Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu pamoja na kamati yake katika Gereza la Mahabusu la Segerea, jijini Dar es Salaam jana.
Mjumbe
wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama, John Chiligati akizungumza na
maofisa wa Jeshi la Magereza wakati kamati hiyo ilipofanya ziara katika
Gereza la Mahabusu la Segerea, jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mussa Azzan Zungu, anayefuata ni Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi.
Kushoto ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma
Malewa.PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.
Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama, Mussa Azzan Zungu
pamoja na wajumbe wa kamati yake wakiwauliza maswali mbalimbali Maafisa
Waandamizi wa Jeshi la Magereza katika Gereza la Segerea lililopo jijini
Dar es Salaam. Kamati hiyo ilitembelea sehemu wanapolala Wafungwa na
Mahabusu, jikoni, ghala la chakula pamoja na kuzungumza na Maafisa wa
Jeshi hilo na baadaye Mahabusu na Wafungwa.
Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mbunge
wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu akizungumza na Mahabusu na
Wafungwa wa Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam (hawapo pichani)
wakati kamati yake ilipofanya ziara ya kikazi katika gereza hilo jana.
Kamati hiyo ilitembelea sehemu wanapolala wafungwa na mahabusu, jikoni,
ghala la chakula pamoja na kuzungumza na Maafisa wa Jeshi hilo na
baadaye Mahabusu na Wafungwa.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi
akiahidi kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali za Mahabusu na Wafungwa
wa Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam (hawapo pichani) walipozitoa
kupitia hotuba yao iliyotolewa wakati Kamati ya Bunge ya Ulinzi na
Usalama ilipofanya ziara katika gereza hilo jana.
Afisa
wa Magereza wa Gereza la Segerea, jijini Dar es Salaam, Gibson
Mwakibibi akiwaonyesha mfuniko wa Hotpot (Chombo cha kuhifadhia chakula)
pamoja na Radio Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama ambapo vifaa hivyo
vinatumika kuficha simu, visu, bangi na vifaa mbalimbali ambavyo ni
hatari kwa usalama wa Mahabusu na wafungwa. Vifaa hivyo vilikuwa
vinaingizwa na mahabusu hao pmaoja na baadhi ya ndugu zao wanapopeleka
chakula gerezani hapo. Hata hivyo, maafisa magereza kwa kutumia chombo
cha kugundulia vifaa mbalimbali (Metal Detector) kinachotumika gerezani
hapo huvikamata vifaa hivyo.
No comments:
Post a Comment