HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, January 19, 2013

Jamaa wa Boda Boda nusura alipue Kituo cha Polisi Jijini Mbeya

Mkazi mmoja  wa Kijiji cha Kiwira wilaya Rungwe mkoani Mbeya,alietambulika kwa jina la Joseph Mwaenga (32) ambae ni mwendesha pikipiki (Bodaboda) anusurika kujilipua na kukilipua kituo  cha Polisi katika mji huo akipinga vitendo vya uonevu vinavyofanywa na askari Kituo hicho.

Kamanda  wa  Polisi  mkoa  wa Mbeya,Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa tukio hilo wakati akizungumza na  wanahabari leo kuwa  tukio  hilo lilimetokea jana majira ya 5 usiku katika  eneo la kituo  hicho .

Alisema  kuwa  kijana  huyo ambae ni mwendesha boda boda alifikishwa  kituoni hapo baada ya  kufanya vurugu katika  kijiwe cha maegesho ya  pikipiki na baada ya hapo alipokonywa pikipiki yake (Boda Boda ) na wananchi na kuifikisha polisi .

Hata  hivyo baada ya kufikishwa kituoni hapo akiwa nje ya  kituo alijimwagia petrol na kumwagia  kituo  cha polisi  kisha kutoa kiberiti na kutaka kujilipua yeye na kituo hicho kabla ya kudhibitiwa na askari  wa  zamu.

Kamanda  Athuman alisema  kuwa mtuhumiwa  huyo baada ya kufanya vurugu  kijiweni  wananchi  walimpokonya  boda boda yake na kuipeleka kituo cha  polisi  na ndipo kijana  huyo alipoamua kuifuata boda boda yake  kituo cha polisi  huku akiwa na dumu la mafuta ya Petrol na kiberiti na baada ya kufika  nje ya kituo hicho alijimwagia mafuta mwili mzima na kumwagia kituo cha  polisi na kisha kutaka  kujitoa muhanga kwa  kujilipua .
 
Alisema  kuwa hakuna madhara yaliyojitokeza kwa binadamu  wala mali juu ya tukio  hilo na mtuhumiwa amekamatwa na atafikishwa mahakamani  wakati  wowote kuanzia  sasa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad