HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 26, 2012

VIONGOZI WA UAMSHO WAPANDISHWA TENA KIZIMBANI LEO

 Mawakili wa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Abdallah Juma kushoto na Salim Tawfik wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu nia yao ya kujitoa kwao siku ya leo katika kesi hiyo kutokana na kile walichoita  usumbufu wanaofanyiwa wateja wao wa kuhangaishwa na kukosa kupelekwa Mahakama ya Kwerekwe kwa muda muafaka 
 Kiongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Sheikh Farid Hadi Ahmed kushoto akiwa na wenzake sita walioletwa Mahakama kuu Zanzibar Vuga wakiwa hawana ndevu na kufunguliwa mashtaka manne mapya mahakamani hapo yakiwemo kuharibu mali za watu zenye thamani ya Shl.Milioni 50 na kufanya vurugu za makusudi zakuhatarisha amani katika nchi
 Baadhi ya Askari wa kutuliza fujo wakiwa Mahakama kuu Zanzibar Vuga kwa lengo la kulinda usalama na  amani Mahakamani hapo
Baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO wakiwa wanatoka katika Mahakama Kuu ya Zanzibar Vuga baada ya kufunguliwa mashtaka manne mapya..Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Na Mohammed Mhina wa Jeshi la Polisi Zanzibar
VIONGOZI wanane wa makundi mawili ya Kiislamu Zanzibar wamefikishwa katika Mahakama Kuu ya Vuga mjini Zanzibar wakituhumiwa na mashitaka manne yanayohatarisha usalama wa taifa.
Waliofikishwa katika Mahakama hiyo ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maimamu mjini Zanzibar Sheikhe Faridi Hadi Ahmedi na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uamsho Sheikhe, Mselem Ali Mselem.
Wengine ni Mussa Juma Issa, Suleiman Juma Suleiman, Azan Khalid Hamdan, Khamis Ali Suleiman, Hassan Bakar Suleiman na Ghalib Ahmada Omar.
Mbele ya Mrajisi wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, George Kazi Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Rayah Mselem alidai katika mahakama hiyo kuwa watuhumiwa wote kwa pamoja wanatuhumiwa kati ya Oktoba 17 na 18 mwaka huu mchana na mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, chini ya kifungu namba 16 kifungu kidogo cha tatu(d) sura ya 47 ya sheria ya Usalama wa Taifa, walitoa lugha ya uchochezi uliosababisha vurugu, ghasia na kuharibu mali yakiwemo majengo na barabara.
Mwendesha mashitaka huyo pia aliendelea kudai mahakamani hapo kuwa, kati ya Mei 26, na Oktoba 19, mwaka huu, Viongozi hao waliwahamasisha wananchi mbalimbali wa mji wa zanzibar na viunga vyake kwa maneno ya uchochezi na kusababisha machafuko yaliyosababisha uhalibifu mkubwa wa mali katika maeneo mbalimbali ya mji wa zanzibar.
Rayah ameyataja maeneo ya mji wa Zanzibar yaliyoathiriwa zaidi na machafuko hayo kuwa ni Lumumba, Msumbiji, Fuoni, Meli Sita na Mbuyuni.
Hata hivyo watuhumiwa hao hawakutakiwa kujibu lolote kutokana na mashitaka yanayowakabili kuwa ni ya kuhatarisha usalama wa taifa.
Pamoja na watuhumiwa hao kudai na kuomba dhamana, mahakama hiyo haikuweza kutoa dhama kutokana na Hati ya iliyowasilishwa mahakamani hapo na Mkurugrnzi wa mashitaka wa zanzibar ya kuzuia dhamana za watuhumiwa hao chini ya kifungu namba 19 kifungu kidogo cha (1) na cha pili (2) sura ya 47 ya Sheria ya Usalama wa Taifa iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande hadi Novemba 8, mwaka huu kesi yao itakapokuja tena kwa kutajwa.
Hiyo ni kesi ya pili kwa watuhumiwa saba na kesi ya kwanza kwa mtuhumiwa hao isipokuwa kwa mtuhumiwa wa nane Ghalib Ahmed Omari ambaye hiyo ni mara yake ya kwanza kufikishwa mahakamani.
Mtuhumiwa Galib ambaye alikuwa akitafutwa na Polisi kwa kuhusika na makosa yaliyompeleka mahakamani, alikamatwa juzi alipoonekana kwenye maeneo ya mahakama ya wilaya ya Mwanakwerekwe kusikiliza kezi za wenzao.
Mara walipoondoka katika ukumbi wa Mahakama kuu ya Vuga, washitakiwa wote saba, walipelekwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe ambako nako jana pia walipaswa kwenda kusikiliza uwamuzi wa au watapatiwa dhama ama vinginevyo.
Hata hivyo mahakama hiyo kesi hiyo imetajwa tu na uwamuzi wa watuhumiwa kupewa au kutopewa dhama katika kesi hiyo ya kwanza utatolewa Novemba 7, mwaka huu.
Watuhumiwa hao wamerudishwa rumande katika Gereza la Chuo cha Mafunzo Ziwani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad