
Waziri wa Afrika Mashariki Mh. Samuel Sitta akipokea heshima ya wimbo wa Taifa baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo kuhudhuria kilele cha maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Mataifa baada ya kutimiza miaka 67 ya UN tangu kuanzishwa.
Mh. Samuel Sitta akikagua gwaride maalum katika kilele cha wiki ya maadhimisho ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Afrika Mashariki akishuhudia upandishwaji wa bendera ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni ishara ya kusheherekea miaka 67 ya Umoja huo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar leo.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou, Mgeni rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meha Jenerali Raphael Muhuga wakiwa Meza kuu.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta akizungumza katika sherehe za kutimiza miaka 67 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa (UN) katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, Sitta aliipongeza Umoja wa Mataifa kwa kuisaidia Tanzania katika nyanja mbalimbali za maendeleo ili kutokomeza umaskini.Waziri Sitta alisisitiza kwamba bado Umoja wa Mataifa unakabiliwa na changamoto nchini kama vile amani na usalama, tatizo la njaa, mabadiliko ya tabia nchi na uwepo wa silaha za maangamizi.Mh. Sitta alifafanua katika kilele cha sherehe hizo umuhimu wa kupitia na kusaidia nchi zinazoendelea kufikia malengo ya millennia.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akitoa nasaha zake wakati wa maadhimisho ya umoja huo katika viwanja vya Karimjee alisema matatizo ya njaa, kupanda kwa bei za mafuta na mtikisiko wa uchumi duniani ni kati ya changamoto kubwa ambazo Umoja wa Mataifa inakabiliana navyo katika dunia ya leo. Dtk Kacou pia aliipongeza Tanzania katika juhudi zake za kupunguza vifo vya wakinamama wakati wa kujifungua na watoto ili waweze kufikia malengo ya millennia itakapofika 2015.Mratibu Mkazi wa UN alisema Tanzania imepunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi mapya ya ugonjwa wa Ukimwi.
Katibu wa UNA Tanzania Fancy Nkuhi akizungumza kwenye hafla hiyo alisema umoja wa mataifa imefanya kazi kubwa katika kuwaunganisha vijana wa bara la Afrika. Nkuhi alisema kupitia YUNA walitoa elimu ya afya ya uzazi na ugonjwa wa Ukimwi kwa vijana katika mikoa kumi hapa nchini Tanzania katika harakati ya kuelimisha vijana madhara ya ugonjwa huo na afya ya uzazi kwa vijana.

Wanafunzi kutoka shule ya mchepuo wa kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium Schools) ambao walikuwa kivutio wakati wa maadhimisho ya miaka 67 ya wiki ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania wakiwa katika gwaride maalum kupamba sherehe hiyo.
Meza kuu ikifurahia jambo wakati wa gwaride la watoto wa shule ya Heritage baada ya kuonyesha mbwembwe katika kupamba sherehe hiyo.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Azania wakitoa burudani ya Wimbo maalum wa kuipongeza UN kutimiza miaka 67 ya kuzaliwa.
Wanafunzi kutoka shule ya mchepuo wa kiingereza ya Heritage (Heritage English Medium Schools) wakiimba wimbo maalum uliobeba ujumbe wa kuhimiza utunzaji wa amani miongoni mwa mataifa wakati wa maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa.


Pichani ni baadhi ya maafisa wa Jeshi waliohudhuria sherehe hizo.

Waziri Sitta akiwa ameambatana na Mwenyeji wake Mratibu Mkazi wa UN Tanzania Dkt. Alberic Kacou (kushoto) wakisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa Kitengo cha maafa UN Bw. Mdathiru Abubakar (wa pili kushoto) akielezea namna ya shirika la Umoja wa Mataifa linavyoshiriki pindi inapotokea maafa nchini. Kulia ni Judith Bihondwa wa UNICEF.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu (kulia) akifafanua utendaji wa kazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake 21 yanavyofanya kazi kwa ukaribu na Serikali ya Tanzania kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samuel Sitta (wa pili kushoto) aliyeambata na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou.
No comments:
Post a Comment