Naibu
  Katibu  Mkuu Mtendaji  Ofisi ya Rais  Kamisheni ya Tume ya Mipango, 
Bw. Clinfford K. Tandari, akifuatilia majadiliano  yaliyohusu  
Utekelezaji wa Mpango wa  Istanmbuli kwa nchi  maskini maarufu kama 
LDGs. Mkutano huo ulifanyika  nchini ya Kamati ya Pili ya Baraza Kuu la 
 67 la Umoja wa Mataifa.
 Alipopata
 nafasi ya kuchangia  utekelezaji wa Mpango huo ( Istambul Plan of 
Action) Bw. Tandari pamoja na mambo mengine, alisema Tanzania imekwisha 
kuuingiza mpango huo katika  Mpango wa Kitaifa wa   Maendeleo wa Kila   
Miaka  Mitano , lengo likiwa ni kuhakikisha kwamba  Tanzania inaondoka 
katika  kundi la nchi maskini na kuingia katika kundi la nchi zenye 
uchumi wa kati ( Middle Income   Countries),  ikifikapo mwaka  2015.
Akabainisha
 kwamba  ili kufikia hatua hiyo, Serikali imejiwekee vipaumbele kadhaa 
ambavyo vimeainishwa katika  Mpango huo wa Miaka mitano.
Akavitaja baadhi ya vipaumbele hivyo kuwa ni  Kilimo na  Usalama wa 
Chakula,   uboreshaji wa huduma za   Elimu,  Afya na  huduma za maji na 
usafi wa mazingira,  maendeleo ya  miundombinu ikiwamo ya barabara, 
reli,  bandari na huduma za nishati. 
Akavitaja
 vipaumbele vingine kuwa ni  usawa wa kijinsia na uwezeshashi pamoja na 
kujenga mazingira bora ya biashara  na ushindaji wa kibiashara.
Katika hatua nyingine  Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Rais 
Kimisheni ya Mipango alieleza kwamba Tanzania ingeweza kufikia lengo 
lake la kutoka katika kundi la nchi maskini na kuwa kundi la nchi ambazo
 uchumi wake ni  wakati  kabla hata ya mwaka 2015 ikiwa tu washirika wa 
 maendeleo ya kichumi watatekeleza ahadi zao za kuisaidia   Tanzania 
zikiwamo zile walizotoa miaka mingi ya nyuma na  ambazo  hazijatekelezwa
 hadi sasa. 
Hata
 hivyo akasema    Tanzania imejidhatiti katika kuhakikisha kwamba 
inaboresha makufanso ya mapato  yake ya ndani ikiwa ni pamoja na kupanua
 wigo wa kodi na kuibua vyazo vipya vya mapato ili kuziba pengo 
litokanalo wa wadau wa maendeleo kushindwa kutekeleza  ahadi zao. 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment