Mgeni rasmi Dk. Mary Mwanjelwa akizindua jarida la shule.
Mkuu wa Shule hiyo, Dk. Binamungu Mukasa akitoa hotuba yake
Mgeni rasmi katika mahali hayo, Dk. Mary Mwanjelwa akitoa hotuba yake
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) mkoa wa Mbeya, Dk. Mary
Mwanjelwa akimkadhi cheti mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri, David Michael
Machuche wakati wa mahafali ya 14 ya Shule ya Sekondari ya Loyola yaliyofanyika
jijini Dar es Salaam.
Mbunge
wa Viti Maalum (CCM) mkoa wa Mbeya, Dk. Mary Mwanjelwa akimkadhi cheti,
Asinta John Mpesa wakati wa mahafali ya 14 ya Shule ya Sekondari ya
Loyola yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mbunge
wa Viti Maalum (CCM) mkoa wa Mbeya, Dk. Mary Mwanjelwa akimkadhi cheti
mwalimu wa shule hiyo, Sista Anastella wakati wa mahafali ya 14 ya Shule
ya Sekondari ya Loyola yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
David Michael Machuche (katikati) akiwa na wahitimu wenzake
Baadhi
ya wahitimu wa Kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Loyola wakiingia
kwenye ukumbi wa mahafali shuleni hapo Mabibo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Habari Mseto Blog)
Baadhi ya wahitimu wa Kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Loyola wakimsikiliza mgeni rasmi wa mahafali ya 14 shuleni hapo.

Baadhi ya wawakilishi wa Chuo cha St. Paul cha London Uingereza wakisikiliza hotuba ya mgeni rasm, Dk. Mary Mwanjelwa (MP)
NA SALUM MKANDEMBA
UONGOZI wa
Shule ya Sekondari ya Loyola, Dar es Salaam, umeshauriwa kuandaa programu
maalum ya kuwasomesha wahitimu wa kidato cha nne katika kipindi cha kusubiri
matokeo ya kujiunga na kidato cha tano.
Ushauri huo
mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mary
Mwanjelwa, katika mahafali ya 14 ya
kidato cha nne shuleni hapo ambako
alikuwa mgeni rasmi.
Mwanjelwa
alisema ili kuwajengea wahitimu hao mazingira ya utayari wa masomo ya kidato
cha tano, kuna haja ya shule kuandaa ratiba itakayowapa wanafunzi masomo hayo,
ili kutopoteza maarifa waliyoyapata shuleni hapo.
Pamoja na
hilo, mbunge huyo aliupongeza uongozi wa
Loyola kwa kuifanya kuwa moja ya shule za kupigiwa mfano nchini na kuwataka
walimu kuhakikisha wanaendelea kulibakisha juu jina la shule hiyo.
Mwanjelwa
akaupongeza uongozi wa shule hiyo chini ya Mkuu wa Shule, Binamungu Mukasa, na
kusema akiwa mmoja wa wazazi wa wahitimu hao 182, anatambua kazi kubwa
inayofanywa na timu nzima ya walimu shuleni hapo katika kuwajenga vijana kielimu,
kiimani na kimaadili.
Katika
hotuba yake, Binamungu aliwashukuru wazazi na kusema mafanikio ya kielimu kwa
wahitimu hao yametokana na juhudi za pamoja za wao (wazazi), walimu na
wanafunzi.
No comments:
Post a Comment