HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 22, 2012

KATIKA KUSHEHEREKEA MIAKA 67 YA UMOJA WA MATAIFA TANZANIA UN FAMILY DAY YAFANA


Kikosi cha timu ya Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja.
Kikosi cha timu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mechi ya Kirafiki kati ya timu ya Umoja wa Mataifa (Blue) na timu ya Wizara ya Mambo ya Nje (Nyeupe) katika UN Family Day ya maadhimisho ya wiki ya Umoja wa mataifa kusheherekea miaka 67 ya Umoja huo zikimenyana kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar.
Austin Makani wa UNHCR (mwenye koti la suti) akiwapa mzuka timu ya Umoja wa Mataifa wakati wa mechi ya kirafiki kusheherekea maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Mataifa ya miaka 67 tangu kuzaliwa kwa shirika hilo.
Hoyce Temu akibadilishana mawazo na baadhi ya wafanyakazi wenzake wakati wa mechi kati ya Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa katika kusheherekea miaka 67 tangu kuzaliwa kwake.
Kiungo wa timu ya Umoja wa Mataifa akijaribu kumtoka kiungo wa timu ya Wizara ya mambo ya nje wakati wa mechi ya kirafiki ambapo timu zote mbili zilitoka sare ya Bao 1-1.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou (katikati) akibadilishana mawazo na baadhi ya Wakuu wa vitengo vya Umoja wa Mataifa wakati wa UN Family day kusheherekea miaka 67 tangu kuzaliwa kwa shirika hilo.
Wakuu wa Vitengo mbalimbali vya Umoja wa Mataifa wakiongozwa na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou (mwenye kofia) wakishindana kuvuta kamba na Wakuu wa vitengo mbalimbali vya Wizara ya mambo ya Nje ambapo UN iliibuka kidedea katika mchezo huo.
Wizara ya Mambo ya Nje walionekana kuwa wengi na wenye fya na kushindwa katika mchezo.
Mchezo wa kushindana kukimbia na magunia kwa wakubwa na wadogo.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou akipozi na Timu ya Wizara ya Mambo ya nje.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akishangaa jambo na wafanyakazi wenzake.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou na Mwakalishi wa UNESCO Tanzania Bi. Vibeke Jensen.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad