Kikosi cha timu ya Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja.
Kikosi cha timu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mechi ya 
Kirafiki kati ya timu ya Umoja wa Mataifa (Blue) na timu ya Wizara ya 
Mambo ya Nje (Nyeupe)  katika  UN Family Day ya maadhimisho ya wiki ya 
Umoja wa mataifa kusheherekea miaka 67 ya Umoja huo zikimenyana kwenye 
viwanja vya Leaders Club jijini Dar.
 Austin 
Makani wa UNHCR (mwenye koti la suti) akiwapa mzuka timu ya Umoja wa 
Mataifa wakati wa mechi ya kirafiki kusheherekea maadhimisho ya wiki ya 
Umoja wa Mataifa ya miaka 67 tangu kuzaliwa kwa shirika hilo.
Hoyce 
Temu akibadilishana mawazo na baadhi ya wafanyakazi wenzake wakati wa 
mechi kati ya Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano 
wa Kimataifa ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa katika 
kusheherekea miaka 67 tangu kuzaliwa kwake.
Kiungo
 wa timu ya Umoja wa Mataifa akijaribu kumtoka kiungo wa timu ya Wizara 
ya mambo ya nje wakati wa mechi ya kirafiki ambapo timu zote mbili 
zilitoka sare ya Bao 1-1.
 Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou 
(katikati) akibadilishana mawazo na baadhi ya Wakuu wa vitengo vya Umoja
 wa Mataifa wakati wa UN Family day kusheherekea miaka 67 tangu kuzaliwa
 kwa shirika hilo.
Wakuu
 wa Vitengo mbalimbali vya Umoja wa Mataifa wakiongozwa na  Mratibu 
Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou (mwenye 
kofia) wakishindana kuvuta kamba na Wakuu wa vitengo mbalimbali vya 
Wizara ya mambo ya Nje ambapo UN iliibuka kidedea katika mchezo huo.
Wizara ya Mambo ya Nje walionekana kuwa wengi na wenye fya na kushindwa katika mchezo.
 Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou akipozi na Timu ya Wizara ya Mambo ya nje.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akishangaa jambo na wafanyakazi wenzake.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Dkt. Alberic Kacou na  Mwakalishi wa UNESCO Tanzania Bi. Vibeke Jensen.
 

 
 















 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment