HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 19, 2012

KAMPUNI YA MEGATRADE YADHAMINI TAMASHA LA JAMBO FESTIVAL


Meneja Masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment Limited,Bw. Goodluck Kway (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 10,Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Jambo Festival ambaye pia ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Idea Afrika ambao ndio waandaaji wa tamasha hilo,Bw.Augustine Namfua kwaajili ya kudhamini Tamasha la Jambo Festival linalotarajiwa kufanyika Oktoba 20 hadi 28 mwaka huu jijini Arusha. 

Na Woinde Shizza,Arusha 

KAMPUNI ya Mega trade Investment kupitia kinywaji chake cha K -Vant Gin wamekabithi kiasi cha hundi ya shs 10 milioni kwa ajili ya kudhamini tamasha la kimataifa la Arusha la sanaa na utamaduni (Jambo Festival litakalofanyika oktoba 20 hadi 28 mwaka huu mkoani Arusha. 

Akizungumza wakati wa kukabithi hundi hiyo ,Meneja masoko wa Megatrade ,Goodluck Kway alisema kuwa tamasha hilo litahusisha wapenzi wa sanaa za mikono,maonyesho, ubunifu na utamaduni kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi. 

Kway alisema kuwa, baadhi ya faida nyingi zitakazopatikana kupitia tamasha hilo ni pamoja na kupandisha hadhi ya jiji la Arusha na kuliweka katika sura mpya na bora zaidi katika ramani ya ulimwengu , kuvutia na kukuza na kuendeleza utalii wa kawaida wa ndani na nje ya nchi. 

Alisema kuwa,tamasha hilo litawezesha kutengeneza nafasi za ajira na biashara kwa vijana, wanawake na wafanyabiashara kwa ujumla kabla, wakati na baada ya tamasha, kutoa nafasi kwa wajasiriamali na wafanyabiashara kushiriki na kufanya biashara katika tamasha hili na maonesho haya, kukuza na kuendeleza utalii wa kitamaduni lakini pia kutoa fursa adimu kwa jamii za Arusha na watanzania kwa ujumla kusherehekea sanaa na utamaduni wao wa asili. 

Kway alisema kuwa, tamasha la Jambo linatarajiwa kuchukua takribani siku tisa likijumuisha shughuli na matukio mbalimbali. 

Naye Afisa Mkuu wa kampuni ya Idea Afrika ambao ndio waandaji wa tamasha hilo, ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha hilo,Augustine Michael Namfua alisema kuwa,amefurahishwa sana na msaada huo kutoka Mega kwani ndio wadhamini wakuu. 

Namfua alisema kuwa,fedha hizo watazitumia kwa umakini uliokusudiwa katika kuhakikisha wamewasadia vijana mbalimbali katika kuibua vipaji vyao na hatimaye tamasha hilo kuwa la mafanikio makubwa. 

Aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi kuja kuinua vipaji vyao katika tamasha hilo kwani hiyo ndiyo fursa pekee ya kuweza kujifunza kupitia kwa wasanii wenzao  

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad