HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 23, 2012

DC AMPA SAA 24 MKUU WA IDARA KUMPA RIPOTI YA MRADI WA MAJI


 Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana akikata utepe kwenye jiwe la msingi wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji uliogharimu kiasi cha zaidi ya shilingi million 5 katika Kijiji cha Bugabu Wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana akifungulia bomba la maji mara baada ya uzinduzi wa mradi wa maji uliogharimu kiasi cha zaidi ya shilingi million 5 katika Kijiji cha Bugabu Wilayani humo.
 Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana akimtwisha ndoo ya maji hayo mmoja wa wanakijiji cha Bugabu Wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana amempa saa 24 Mkuu wa Idara ya Maji wa wilaya hiyo kuwasilisha ripoti ya mradi wa maji uliojengwa katika Kijiji cha Bugabu uliofadhiriwa na kampuni ya Alpha Choice ya Mwanza. 

Amri hiyo ya Liana inatokana na malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Bugabu wakati wa uzinduzi wa mradi huo wa maji uliogharimu kiasi cha zaidi ya shilingi million 5. Akizungumza muda mfupi baada ya kuzindua mradi huo wa maji utakaosaidia wananchi wa vijiji vitatu, Jaqueline Liana amesema kumekuwa na tabia kwa wakuu wa idara na viongozi wa vijiji kutosoma mapato na matumizi ya miradi.

 Amesema kuwepo kwa usiri katika miradi mbalimbali kunawafanya wananchi kuichukua serikali yao,kitu ambacho kinaweza kuepukwa iwapo suala la kusomwa mapato na matumizi litazingatiwa. 

Afisa mtendaji wa kijiji cha Bugabu Rebecca Jonas na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamezungumzia changamoto mbalimbali kuhusiana na mradi huo wa maji Meneja mauzo wa Kampuni ya Alpha Choice inayomiliki viwanda vya kusindika minofu ya samaki katika nchi za Afrika Mashariki Bruno Mhoja amesema mradi huo wa maji ni makakati wa kampuni kushirikiana na jamii katika miradi ya maendeleo. 

Mradi huo wa maji ni wa kwanza katika kijiji cha Bugabu kutolewa na wawekezaji ambao utawanufaisha wananchi zaidi ya laki moja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad