HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 13, 2012

BONDIA THOMAS MASHALI NA MEDY SEBYALA WA UGANDA WAPIMA UZITO KWA AJILI YA MPAMBANO WAO KESHO JUMAPILI

Bondia THOMAS MASHALI kushoto akitunishiana misuri na MEDY SEBYALA wa UGANDA mara baada ya kupima uzito jijini Dar es salaam leo kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika kesho ikiwa ni siku ya kumbukumbu ya baba wa Taifa (Mwl. Julius K. Nyerere) katika pambano la Ubingwa wa Africa mashariki litakalofanyi ukumbi wa Friends corner hotel.anaeshudia katikati ni Rais wa TPBC Onesmo Ngowi ambaye ndie msimamizi mkuu wa mpambano huo.
Bondia MEDY SEBYALA wa UGANDA akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na THOMAS MASHALI litakalofanyika kesho katika ukumbi wa Friends corner hotel pambano la Ubingwa wa Africa mashariki.
Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na jonas Segu kulia utakaofanyika kesho.

Bondia Jonas Segu akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kulia mpambano huo wa mabondia chipkizi umevuta hisia za watu wengi kwa upande wa wapenzi wa mchezo wa masumbwi nchini.
Bondia Jonas Segu kushoto na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakitunishiana misuri baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika kesho katika ukumbi wa Friends Corner,jijini Dar.picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad