HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 24, 2012

Benki ya KCB Tanzania yasaidia vifaa vya mama na mtoto kwa hospitali za Temeke na Buguruni

 Matroni wa Haopitali ya Temeke jijini Dar es Salaam, akitoa  ukaribisho kwa wageni mbalimbali waliofika katika hafla ya kupokea  msaada wa vifaa mbalimbali vya Hospitali ya Temeke na Buguruni
 Vilivyotolewa na Benki ya KCB Tanzania vikiwa na thaman ya shilingi  milioni 17,152,000.
 Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro,akisalimiana na wauguzi wa hospitali za Temeke na Buguruni wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa vifaa mbalimbali vya hospitali hizo wenye thamani ya shilingi milioni 17,152,000.
Wauguzi wa hospitali ya temeke wakifurahia msaada wa mashine ya  joto inayosaidia watoto wachanga waliozaliwa kabla ya mda wake Njiti,  baada ya kukabidhiwa msaada na benki ya KCB.
Wafanyakazi wa benki ya KCB Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wa  Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro, wakiwa katika picha ya  pamoja na wafanyakazi wa Hospitali ya Temeke na Buguruni zote za  jijini Dar es Salaam, baada ya KCB kukabidhi Msaada wa vifaa  mbalimbali kwa hospitali hizo wenye thamani ya shilingi Milioni  17,152,000.
Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro,(kulia) akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Temeke jijini  Dar es Salaam, DR.Amani Malima msaada wa Folding Screens  moja kati ya 3 zilizotolewa msaada na benki hiyo ikiwemo vitu  mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 11,152,000 ka ajili ya  hospitali hiyo. (Kulia) Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Temeke  James Magoti.
  Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura  Muro,(kulia) akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Buguruni  jijini Dar es Salaam, DR.Hawa Lesso msaada wa mashini ya joto  inayosaidia kutunzia motto aliyezaliwa kabla ya wakati wake (NJITI)  katika hafla iliyofanyika Hospitali ya Temeke, Benki ya KCB ilitoa  vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi Milioni 17,152,000.  Wanaoshuhudia ni wauguzi wa ahaospitali ya Buguruni waliofika kupokea  msaada huo.
Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro,(kulia) akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Temeke jijini  Dar es Salaam, DR.Amani Malima,mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumulia
wakati wa hafla ya kukabidhiwa vitu mbalimbali kwa ajiri ya Hospitali  ya Temeke na Buguruni vyenye thamani ya shilingi Milioni  17.152.000.(katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Temeke James
 Magoti.
Benki ya KCB Tanzania, imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kusaidia afya ya mama na mtoto vyenye thamani ya shilingi 17,152,000/- kwa hospitali za Temeke na Buguruni zilizopo jijini Dar es Salaam Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Benki ya KCB Tanzania, imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kusaidia afya ya mama na mtoto vyenye thamani ya shilingi 17,152,000/- kwa hospitali za Temeke na Buguruni zilizopo jijini Dar es Salaam Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Mkurugenzi wa bodi ya benki hiyo Zuhura Muro alisema katika kuhadhimisha wiki ya jamii mwaka huu benki ya KCB imeamua kuelekeza misaada yake katika sekta ya afya “Wakati wa wiki ya jamii mwaka jana na juzi tulitoa madawati na vitabu kwa shule mbalimbali nchini. 

Mwaka huu tumechagua kusaidia sekta ya afya hasa kwa upande wa akinamama na watoto ili kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na uhaba wa vifaa muhimu hospitalini,” “Mkurugenzi huyo wa bodi alisema benki ya KCB inaatambua umuhimu wa afya ya mama na mtoto na ndiyo maana tumeona ni jambo zuri kuwekeza katika sekta ya afya. Nikiwa kama mama ninayo furaha kwa kuwa naamini msaada huu utaweza kuokoa maisha ya akina mama na watoto,” alieleza.

 Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya Temeke Amani Malima alisema kuwa hospitali yake imekuwa ikihudumia akina mama wengi kuliko uwezo wake kutokana ukosefu wa vifaa. “Tunapokea akina mama wengi wanaokuja kujifungua zaidi ya uwezo wetu. Wengine huwa wanazaliwa wakiwa bado hawajatimia na hulazimika kuwapa rufaa ya kwenda hospitali nyingine kama Muhimbili kutokana na kutokuwa na vifaa. Tunaishukuru benki ya KCB kwani msaada huu utasaidia kuboresha hali,” alisema.

Naye mganga mfawidhi wa hospitali ya Buguruni Dr Hawa Lesso aliishukuru benki ya KCB na kusema kuwa utasaidia kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa kabla wakiwa hawajatimia (pre mature). Watoto wanaozaliwa kabla ya kutimia wakati mwingine hupoteza maisha kabla ya kuwapa rufaa ya kwenda hospitali nyingine kutokana na ukosefu wa vifaa. Tunaishuru benki ya KCB kwani imesikiliza kilio chetu, Tunaomba taasisi nyingine za kifedha kuiga mfanio wa benki ya KCB. 

 Vifaa vilivyotolewa kwa hospitali ya Temeke ni pamoja na mashine moja ya joto kwa watoto waliozaliwa bila kutimia (Incubator), Folding screens 10, seti ya mashine ya hewa 3 (Oxygen flow meter) na sare za wauguzi pea 10 vyote vikiwa na thamani ya shilingi 11,252,00/- Hospitali ya Buguruni ilipokea mashine moja ya joto kwa watoto waliozaliwa bila kutimia yenye thamani ya shilingi 5,900,000/-

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad