Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mh. William Lukuvi (Mb) akisoma hotuba yake iliyo sisitiza Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa mfano katika kupunguza matumizi ya Serikali, wakati alipofungua kikao cha Baraza la Wafanyakaazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu katika Ukumbi wa Ofisi hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya waziri Mkuu wakimsikililiza Waziri Lukuvi (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakaazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, ambapo Lukuvi aliwataka wajumbe kuwa na nidhamu ya fedha zilizo idhinishwa kwa matumizi ya Ofisi.
Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mh. William Lukuvi (Mb), (wa nne kutoka kushoto ) akiwa na Viongozi pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu muda mfupi baada ya kufungua kikao cha baraza hilo katika Ukumbi wa Ofisi hiyo jijini Dar es Salaam leo, (wa nne kulia) ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo.
No comments:
Post a Comment