HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 29, 2012

ZIARA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR KATIKA KANISA LILILOCHOMWA MOTO

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohamed Aboud akielezea jambo kwa Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Zanzibar Dickson D,Kaganga wakwanza kulia kuhusiana na kuchomwa moto kwa Kanisa hilo liliopo Kariakoo Mjini Zanzibar katikati ni Mkuu wa Jeshi la Polisi I,G,P Saidi Mwemwa.
Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Zanzibar Dickson D,Kaganga akielezea kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mohamed Aboud na Viongozi wengine mbalimbali kile kilichotokea baada ya Kanisa hilo kuchomwa motokatika Vurugu zilizotokea Zanzibar ambapo hadi sasa watu 30 wamekamatwa na baadhi yao kuhusishwa na tokeo hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar Abdalla Mwinyi Khamis akitoa hotuba na kuonyesha Umoja na Mshikamano uliokuwepo kati ya Waislam na Wakristo kwa Picha ambayo imebuniwa na Mchoraji wa kingereza na kuwataka kuendelea na mshikamano wao ili kuzidi kuleta amani nchini.
Mkuu wa Jeshi la Polisi I,G,P Saidi Mwema akitoa hotuba kwa Maaskofu na baadhi ya waumini wa Kikristo katika kanisa la Tanzania Assemblies of God Zanzibar lililochomwa moto,ambapo hadi sasa watu 30 wamekamatwa na baadhi yao kuhusishwa na tokeo hilo.kuliani kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Abdalla Mwinyi na kushoto yake ni Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Mussa Ali Mussa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohamed Aboud akitoa hotuba katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God Zanzibar kufuatia fujo zilizotokea Zanzibar na kusababisha Kuchomwa moto kwa Kanisa hilo, hapo katika ukumbi wa Kanisa hilo Kariakoo Mjini Zanzibar.hadi sasa watu 30 wamekamatwa na baadhi yao kuhusishwa na tokeo hilo.
Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Zanzibar Dickson D,Kaganga akimuonesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud maeneo yalioathirika zaidi baada ya Kanisa hilo kuchomwa moto katika Vurugu zilizotokea Zanzibar ambapo hadi sasa watu 30 wamekamatwa na baadhi yao kuhusishwa na tokeo hilo.
Mkuu wa Dini ya Kiislam Afisi ya Mufti wa Zanzibar Thabit Noman Jongo akitoa hotuba ya Dini inavyoeleza kuhusiana na kudumisha Amani na Usalama katika nchi na kuondosha mifarakano na chuki na kuharibu mali.Katika kanisa la Tanzania Assemblies of God Zanzibar ambalo limechomwa moto.Picha na Idara ya Habari Maelezo- Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad