Rais Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Kanali Pastory Kamugisha wa JWTZ aliyefariki juzi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao mkoani Kagera. Shughuli hii imefanyika leo katika kambi ya jeshi ya Lugalo Jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Kamishana wa Magereza,Marehemu Elias Mtige Nkuku, aliyefariki juzi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao mkoani Singida. Shughuli hii imefanyika leo katika bwalo la jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es salaam.Picha na IKULU.
No comments:
Post a Comment