HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 1, 2011

Wanafunzi Chuo Kikuu Eckernforde wagoma

wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Eckernforde Tanga Univesity kilichopo Jijini Tanga, wakimzonga Mshauri wa wanafunzi wa chuo hicho 'Dean Of Students' Bw Zawadiel Mkilindi kufuatia mzozo mkubwa ulioibuka chuoni hapo kuhusu kusimamishwa masomo wanafunzi 11 ambao walikosa mkopo kutoka bodi ya mikopo hivyo uongozi wa chuo kuwapa barua ya kuwataka kuondoka chuoni hapo.
Makamo wa rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Eckernforde Tanga Univesity Bw Santus Tangatya akiwasomoea wanafunzi wenzake barua ambayo wanafunzi 11 waliokosa mikopo ya bodi ya mikopo wakitakiwa kundoka chuoni hapo licha ya wanafunzi wenzao kuwachangia sehemu ya mikopo hiyo ili waendelee kubaki lakini uongozi wa chuo uling'ang'ania kutaka kuondoka.
"Tumechanga shilingi 100,000 kila mtu ili wezetu waziondoke chuoni lakini uongozi wamegoma na wameona barua hii eti wenzetu 11 waondoke, sisi kama viongozi wenu mliotuchagua tunasema hatukubali na hatutaingia darasani hadi hatma ya wenzetu hawa ambao wamewalazimisha warudie mwaka kwasababu ya kukosa mikopo, hawakubali wametumia ubabe tu," Makamo wa rais wa serikali ya chuo kikuu cha Eckernforde tanga univesity Bw. Santus Tangatya akiwaeleza wanafunzi wenzake waliokusanyika kwenye bustani za chuo hicho.
Mshauri wa wanafunzi "Dean Of Students' Bw. Zawadiel mkilindi wa kwanza kushoto akitoa maelezo ni kwanini uongozi wa chuo cha Eckernforde Tanga Univesity umewapa barua za kuwataka kurudia mwaka wanafunzi 11 kati ya 64 wa mwaka wa pili wanaochukua shahada ya elimu kufuatia kukosa mikopo kutoka bodi ya mikopo nchini, lakini hata hivyo wanafunzi hao hawakukubaliana na maelezo yake.Picha na Mashaka Mhando,Tanga

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad