Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (wa tatu kushoto) akipokea sehemu ya misaada iliyotolea na Umoja wa Masheikh na Wanazuoni wa Nchini Tanzania wenye jumla ya thamani ya sh. Milioni 12,kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja huo,Sheikh Hamis Mataka (mwenye kanzu nyeusi) leo kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.Wengine pichani ni wajumbe wa Umoja huo wa Masheikh.
Katibu
Mkuu wa Umoja wa Masheikh na Wanazuoni Nchini,Sheikh Hamis Mataka
(katikati) akisoma taarifa fupi ya misaada mbali mbali iliyotolewa na
umoja huo kwa ajili ya waathirika wa janga la Mafuriko lililolikumba
jiji la Dar es Salaam hivi karibuni wakati walipofika kwenye ofisi ya
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (wa pili kulia) leo
kwa ajili ya kukabidhi msaada huo.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq akitoa shukrani kwa wale
woote waliofika ofisini kwake leo kwa lengo la kuwasilisha midaada
mbalimbali kwa ajili wa waathirika wa Mafuriko yaliyotokea hivi karibu
jijini Dar.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (kulia) akipokea Misaada ya vyakula kutoka kwa vijana wanaounda Muungano wa Mashirika ya Vijana nchini,Kushoto ni Kiongozi wa Muundano huo,Nyakia Ally na Katikati ni Mjumbe wa Muungano huo,Sostenes Mitti.
Kiongozi wa Muungano wa Mashirika ya Vijana nchini,Nyakia Ally (kushoto) akiongea na vyombo vya habari wakati wa kukabidhi sehemu ya misaada kwa ajili ya waathirika wa Mafuriko jijini Dar es Salaam wakati walipofika kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (kulia) kukabidhi misaada yao hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadiq (kushoto) akisikiliza kwa makini taarifa ya Meneja Mauzo wa DarBrew LTD ambao ni Watengenezaji wa Kinywaji cha Chibuku,Urban Shayo wakati walipofika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kukabidhi Msaada wao kwa waathirika wa Mafuko.
No comments:
Post a Comment