HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 12, 2011

BALOZI SEFUE,NAIBU BALOZI MAMA MUNANKA WAGENI SHEREHE ZA MIAKA 50 YA UHURU,NEW YORK

Mh.Balozi Ombeni Sefue ambae ni Balozi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa New York akiongea na Watanzania wa New York katika kusherehekea miaka 50 ya UHURU,Tanzania Bara iliyofanyika Jumamosi December 10,2011,mjini humo.
 
Mh.Naibu Balozi wa Tanzania Nchini Marekani na Mexico,Mama Munanka,akiongea machache kwa niaba ya Balozi Mh.Mwanaidi Maajar ambae hakuweza kuhudhulia sherehe hizi za miaka 50 ya UHURU kutokana ya Yeye kuwepo Tanzania.
 Balozi wetu wa kudumu Umoja wa Mataifa,New York,Mh.Ombeni Sefue(shoto mwenye miwani) akiingia ukumbini kujumuika na Watanzania wa New York katika sherehe za Miaka 50 ya UHURU iliyofanyika Jumamosi December 10,2011 kulia ni Mh.Naibu Balozi Mama Munanka.
 Balozi wa kudumu waTanzania umoja wa mataifa New York,Mh. Ombeni Sefue(shoto) akisindikizwa na mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania New York,Bw, Hajji Khamis alipokua akiingia ukumbini hapo.
 Balozi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa,New York,Mh.Ombeni Sefue akipiga picha ya pamoja na Balozi wa Somalia katika sherehe za miaka 50 ya UHURU,Tanzania Bara zilizofanyika New York Jumamosi December 10,2011
kutoka shoto ni Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini,Mh. Balozi Ombeni Sefue,Balozi wa Somalia akiwa pamoja na mkwewe wakipata picha ya kumbukumbu katika sherehe za miaka 50 ya UHURu Tanzania Bara zilizofanywa na Jumuiya ya Watanzania New York.
 Mh.Blalozi Ombeni Sefue(wapili toka shoto) akiwa pamoja na Mkewe(kati mwenye nguo nyeusi) Mh,Naibu Balozi wa Tanzania Nchini Marekani,Mama Munanka(wapili toka kulia) wakiwa meza kuu na viongozi wa Jumuiya ya Watanzania wa New York katika kusherehekea miaka 50 ya UHURU Tanzania Bara ilyofanyikia katika Ukumbi wa Malcolm X,Manhattan,New York,Jumamosi December 10,2011
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya wa Tanzania New York,Bw,Hajji Khamis akisema machache kuhusiana na miaka 50 ya UHURU kabla hajamkaribisha Mh.Balozi Ombeni Sefue.
 Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania New York ukipiga picha ya pamoja na Balozi Sefue,Mkwewe na Naiibu Balozi wa Tanzania Nchini Marekani Mama Munanka.
 Mh.Balozi Ombeni Sefue pamoja na Mkewe katika picha ya pamoja na Uongozi wa Jumuiya ya Watzanzania,New York na wadhamini wa sherehe hiyo ya miaka 50 ya UHURU iliyofanyikia katika ukumbi wa Malcolm X,Manhattan,New York,Jumamosi Decenber 10,2011.
 Juu na chini ni  Mh.Balozi Sefue pamoaja na Mkewe wakipiga picha ya pamoja na Watanzania waliojumuika pamoja katika kusherehekea miaka 50 ya Uhuru New York,NY.
 Mh.Naibu Balozi wa Tanzania Nchini Marekani na Mexico,Mama Munanka akiwa anajisaidia mwenyewe kupata maakuli katika sherehe za miaka 50 ya UHURU wa Tanzania Bara zilizofznyika New York kushoto ni Balozi wa Somalia akiwa na mkwewe(kati)
 Balozi wa Somali(kulia) akiwa na mwenyeji wake Mh,Balozi Ombeni Sefue wakijisaidia kupata maakuli katika sherehe za miaka 50 zilizofanyika New York,NY Nchini Marekani.
Mh.Balozi Sefue akiendelea kujipakulia Maakuli

1 comment:

  1. Jamani mkiandika habari hebu fanyeni uchunguzi kabla hamjachapisha. huyo mlomuandika balozi wa Somali na mkwewe, sio sawa. ni Bwana Duale na mkewe Bibi Ashura na wote ni Watanzania

    ReplyDelete

Post Bottom Ad