
Hii ilikuwa mwaka 1992 siku Yanga ilipofanya mauaji kwa mnyama uwanja wa Taifa (sasa wa Uhuru) Dar kwa goli la shuti la mbali la nahodha Ken Mkapa lililomshinda Mwameja.
Nakumbuka mechi hii ilichezwa siku chache baada ya Yanga kutoka Misri ilikokwenda menyana na Ismailia na kutoka sare ya 1-1.
Pichani ni baadhi ya wanaume wa shoka wa Yanga. Toka kushoto ni Hamis Gaga 'Gagarino'(marehemu), Saidi Mwamba 'Kizota(marehemu), David Mwakalebela, Method Mogella(marehemu), Abeid Mziba, Ken Mkapa, Na Salum Kabunda 'Ninja'. Nyuma kwa mbali ni Stephen Nemes.
Vizazi hivi sijui kama vitakuja tokea tena! Mungu ibariki Tanzania. Wenye kumbukumbu zaidi za mechi hii tukumbushane...
nawasilisha
mdau
Nathan Mpangala
No comments:
Post a Comment